Thursday, November 16, 2023

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA MAWAZIRI KUHUSU USALAMA WA BAHARI YA HINDI

Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Suleiman Masoud Makame ameongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Tatu wa Mawaziri kuhusu Usalama na Ulinzi wa Bahari  Magharibi mwa Bahari ya Hindi uliofanyika Balaclava nchini Mauritius tarehe 16 Novemba 2023.

 

Mkutano huo ambao umeandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Biashara za Kimataifa ya Mauritius kwa kushirikiana na Kamisheni ya Bahari ya Hindi, pamoja na mambo mengine ulipokea taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya mikutano ya aina hiyo iliyofanyika mwaka 2018 na 2019 pamoja na kujadili hatua za kuchukua ili kuimarisha ulinzi na usalama wa bahari. 

 

Kadhalika, wakati wa Mkutano huo, Nchi mbalimbali, Mashirika ya Kimataifa na kikanda na wadau wa maendeleo zilipitisha  Azimio la Pamoja  kuhusu umuhimu wa  ushirikiano  na nguvu ya pamoja katika kulinda watumiaji wa Bahari ya Hindi dhidi ya changamoto mbalimbali zinazotokana na matumizi ya bahari ikiwemo ongezeko la makosa yanayovuka mipaka, uharamia na uvuvi haramu.

 

Ujumbe wa Tanzania ulimjumuisha pia Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Rosemary Jairo, Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania nchini Mauritius, Bw. Marday Venkatasamy na Maafisa Waandamizi kutoka Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania na Ubalozi wa Tanzania nchini Zimbabwe ambao unawakilisha pia nchini Mauritius.

Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi wa Zanzibar, Mhe. Suleiman Masoud Makame (wa pili kulia) akishiriki Mkutano wa Tatu wa Mawaziri kuhusu Usalama na Ulinzi wa Bahari Magharibi mwa Bahari ya Hindi uliofanyika Balaclava nchini Mauritius tarehe 16 Novemba 2023. Mhe. Makame aliongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo.
Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Suleiman Masoud Makame (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania nchini Mauritius, Bw. Marday Venkatasamy.  Mhe. Makame aliongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Tatu wa Mawaziri kuhusu Usalama na Ulinzi wa Bahari  Magharibi mwa Bahari ya Hindi uliofanyika Balaclava nchini Mauritius tarehe 16 Novemba 2023.

Waziri wa Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Suleiman Masoud Makame (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania nchini Mauritius, Bw. Marday Venkatasamy, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano  wa Afrika Mashariki, Bi. Rosemary Jairo (wa pili kulia) na Afisa kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Zimbabwe ambao unawakilisha pia Mauritius, Bi. Gwantwa  Mwaisaka wakati wa  Mkutano wa Tatu wa Mawaziri kuhusu Usalama na Ulinzi wa Bahari  Magharibi mwa Bahari ya Hindi uliofanyika Balaclava nchini Mauritius tarehe 16 Novemba 2023.

Mhe. Makame (wa nne kulia waliosimama) katika picha ya pamoja na Viongozi wengine walioshiriki Mkutano wa Tatu wa Mawaziri kuhusu Usalama na Ulinzi wa Bahari  Magharibi mwa Bahari ya Hindi uliofanyika Balaclava nchini Mauritius tarehe 16 Novemba 2023.



 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.