Monday, November 13, 2023

WAZIRI MAKAMBA AWASILI UHOLANZI KWA ZIARA YA KIKAZI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akielezea juu ya ushiriki wa ujumbe wa Tanzania katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uholanzi litakalofanyika tarehe 14 na 15 Novemba 2023 jijini The Hague, Uholanzi. Kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Dkt. Tausi Kida na kushoto ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano waTanzania nchini Uholanzi, Mhe. Caroline Chipeta.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Yusuf Makamba (Mb.) amewasili Jijini The Hague, Uholanzi kwa ziara ya kikazi ya siku tatu (3) kuanzia tarehe 13 - 15 Novemba 2023. 

Pamoja na mambo mengine, Mhe. Makamba ataongoza ujumbe wa Tanzania katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji Kati ya Tanzania na Uholanzi litakalofanyika tarehe 14 na 15 Jijini The Hague.

Aidha, pembezoni mwa kongamano hilo, Mhe. Waziri Makamba atapata nafasi ya kukutana na Waziri mwenzake wa Mambo ya Nje wa Uholanzi, Mhe. Kanke Bruins Slot. Kadhalika, Mhe. Makamba anatarajiwa pia kukutana na kufanya mazungumzo na Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Uholanzi (Tanzania Diaspora).

Waziri Makamba ameambatana na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Kida na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Daniel Mushi. Wengine wanaoshiriki kwenye ujumbe wa Mhe. Waziri ni Mabalozi na Maafisa Waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Pamoja na Wakuu wa Mashirika mbalimbali Serikalini yanayotafuta ubia na mashirika ya Uholanzi. 

Aidha ujumbe wa Waziri Makamba umehusisha wafanyabiashara 16 kutoka sekta binafsi za Tanzania ambao wanashiriki kwenye kongamano hilo.
Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Biashara za Kimataifa na Diplomasia ya Uchumi, Balozi John Ulanga akifafanua masuala mbalimbali yatakayojiri wakati wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uholanzi kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (kushoto) na kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya mifugo), Dkt. Daniel Mushin a wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga.
Viongozi Waandamizi kutoka sekta ya umma na binafsi walioambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) nchini Uholanzi wakifatilia ufafanuzi wa masuala mbalimbali katika kikao cha ndani cha maandalizi.
Viongozi Waandamizi kutoka sekta ya umma na binafsi walioambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) nchini Uholanzi wakifatilia ufafanuzi wa masuala mbalimbali katika kikao cha ndani cha maandalizi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Caroline Chipeta mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Amsterdam, Uholanzi tarehe 13 Novemba 2023
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akielezea juu ya ushiriki wa ujumbe wa Tanzania katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uholanzi litakalofanyika tarehe 14 na 15 Novemba 2023 jijini The Hague, Uholanzi. Kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Dkt. Tausi Kida na kushoto ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano waTanzania nchini Uholanzi, Mhe. Caroline Chipeta

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.