Friday, November 24, 2023

NAIBU WAZIRI BYABATO AKUTANA NA NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA JAMHURI YA KOREA

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea, Bi. Oh Youngju walipokutana kwa mazungumzo pembezoni mwa Mkutano wa 23 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha.


Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato, amekutana na kuzungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea, Bi. Oh Youngju, pembezoni mwa Mkutano wa 23 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Jamhuri ya Korea kwa manufaa ya pande zote mbili.

Akizungumza katika mkutano huo Naibu Waziri Mhe. Byabato alimuelezea Bi. Youngju kuridhishwa kwa Tanzania juu ya ushirikiano na uhusiano uliopo kati yake na Jamhuri ya Korea na kuahidi kuendelea kushirikiana na nchi hiyo kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili.

Naye Bi. Youngju alimuelezea Naibu Waziri Byabato juu ya mpango wa Jamhuri ya Korea wa kuandaa Mkutanoo kati ya Nchi yake na Viongozi wa Bara la Afrika uliopangwa kufanyika mapema mwezi Juni 2024 na kwamba anaialika rasmi Tanzania ishiriki katika mkutano huo.
 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato akimsikiliza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea, Bi. Oh Youngju walipokutana kwa mazungumzo pembezoni mwa Mkutano wa 23 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha.
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea, Bi. Oh Youngju yaliyofanyika pembezoni mwa Mkutano wa 23 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha.
Mazungumzo yakiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.