Thursday, November 30, 2023

TANZANIA NA VENEZUELA KUIMARISHA USHIRIKIANO


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akisalimiana na Balozi wa Venezuela nchini mwenye makazi yake jijini Nairobi, Kenya, Mhe. Jesus Manzanilla Puppo walipokutana kwa mazungumzo katika ofisi za Wizara jijini Dodoma

Serikali ya Tanzania na Venezuela zimeahidi kuendeleza ushirikiano wa kidiplomasia uliopo baina ya nchi hizo ili kufungua maeneo mapya ya ushirikiano kwa manufaa ya pande zote.

Ahadi hiyo imetolewa katika mazungumzo kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo na Balozi wa Venezuela nchini mwenye makazi yake jijini Nairobi, Kenya, Mhe. Jesus Manzanilla Puppo walipokutana katika ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Mazungumzo ya viongozi hao yalijikita katika kuimarisha ushirikiano kwenye sekta za nishati hususan mafuta na gesi, kukuza teknolojia na maendeleo ya miji, elimu na utamaduni.

Pia, kupitia mazungumzo hayo Balozi Shelukindo amewakaribisha wawekezaji kutoka Venezuela kuja kuwekeza katika sekta za utalii, viwanda, madini, afya na kilimo.

Vilevile, kupitia mazungumzo hayo wamependekeza kuanzishwa kwa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Venezuela, ambapo Tanzania itakuwa mwenyeji wa mkutano huo utakaokubaliwa kati ya pande mbili.
Mazungumzo yakiendelea
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akimsikiliza Balozi wa Venezuela nchini mwenye makazi yake jijini Nairobi, Kenya, Mhe. Jesus Manzanilla Puppo walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Venezuela nchini mwenye makazi yake jijini Nairobi, Kenya, Mhe. Jesus Manzanilla Puppo yaliyofanyika jijini Dodoma

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.