Friday, November 24, 2023

RAIS SAMIA ASHIRIKI MAJADILIANO YA JUU YA MABADILIKO YA TABIA NCHI NA USALAMA WA CHAKULA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifafanua jambo kwenye Mkutano wa Majadiliano ya Juu kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula uliofanyika jijini Arusha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameungana na Rais wa Kenya Mhe. William Ruto na Rais wa Burundi Mhe. Evereste Ndayishimiye kushiriki Mkutano wa Majadiliano ya Juu kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula uliofanyika jijini Arusha.

Mkutano huo wa ngazi ya juu wa majadiliano uliandaliwa na Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ukiwa ni mkutano wa pembezoni kuelekea Mkutano wa 23 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika terehe 24 Novemba 2023.

Majadiliano hayo yalikuwa na kauli mbiu isemayo kuongeza Ustahimilivu wa Mabadiliko ya Tabia Nchi kwa usalama wa chakula na mazingira endelevu kwa Ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 

Mkutano huo wa Majadiliano ya Juu ulilenga kupata msimamo wa pamoja wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki maalum kwa ajili ya Mkutano wa 28 wa Nchi Wanachama wa Mikataba wa Umoja wa Matanda kuhusu Mabadiliko Tabianchi (COP28) utakaofanyika kuanzia tarehe 30 Novemba hadi 12 Disemba 2020 mjini Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu

Msimamo huo wa pamoja unatarajiwa kupitishwa katika Mkutano wa 23 wa kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika tarehe 24 Novemba 2023 jijini Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifafanua jambo kwenye Mkutano wa Majadiliano ya Juu kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula uliofanyika jijini Arusha
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akifuatilia Mkutano wa Majadiliano ya Juu kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula uliokuwa ukiendelea jijini Arusha
Balozi wa Tanzania nchini Kenya Mhe. Balozi Dkt. Bernard Kibesse akifuatilia Mkutano wa Majadiliano ya Juu kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula uliokuwa ukiendelea jijini Arusha
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Balozi Stephen P. Mbundi akifuatilia Mkutano wa Majadiliano ya Juu kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula uliokuwa ukiendelea jijini Arusha
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akifurahia jambo na Rais wa Jamhuri ya Kenya William Ruto alipowasili kwenye Mkutano wa Majadiliano ya Juu kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula uliofanyika jijini Arusha
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akifuatilia Mkutano wa Majadiliano ya Juu kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula uliokuwa ukiendelea jijini Arusha
Rais wa Jamhuri ya Kenya William Ruto akisisitiza jambo kwenye Mkutano wa Majadiliano ya Juu kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula uliofanyika jijini Arusha
Rais wa Jamhuri ya Burundi Mhe. Evereste Ndayishimiye na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki akisisitiza akitoa hotuba ya ufunguzi wa Mkutano wa Majadiliano ya Juu kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula uliofanyika jijini Arusha
Mkutano wa Majadiliano ya Juu kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula ukiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.