Thursday, November 23, 2023

BALOZI NAIMI AWASILISHA HATI KWA RAIS WA AUSTRIA

 

Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Austria na katika Ofisi za Umoja wa Mataifa Vienna, Mhe. Naimi S. Aziz (kulia) akiwasilisha  Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Austria, Mhe. Alexander Van Der Belen (kushoto) tarehe 21 Novemba, 2023


Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Austria na katika Ofisi za Umoja wa Mataifa Vienna, Mhe. Naimi S. Aziz (kulia) akizungumza na Rais wa Jamhuri ya Austria, Mhe. Alexander Van Der Belen (kushoto) baada ya kuwasilisha  Hati za Utambulisho tarehe 21 Novemba, 2023

Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Austria na katika Ofisi za Umoja wa Mataifa Vienna, Mhe. Naimi S. Aziz akikagua gwaride maalum alipowasili Ikulu jijini Vienna kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Austria tarehe 21 Novemba, 2023

 

 

Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Austria na Katika Ofisi za Umoja wa Mataifa Vienna, Mhe. Naimi S. Aziz amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Austria, Mhe. Alexander Van Der Belen tarehe 21 Novemba, 2023.

Baada ya kuwasilisha Hati hizo za utambulisho Serikali ya Jamhuri ya Austria ilimuahidi ushirikiano Mhe. Balozi  Aziz kwa kipindi chote atakachohudumu katika kituo hicho na kumuwezesha kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na hivyo kuendelea kuimarsiha uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Austria.

Naye Mhe. Balozi Aziz alishukuru na kuahidi kushirikiana na Serikali ya Austria katika utekelezaji majukumu yake na kuhakikisha uhusiano kati ya Tanzania na Austria unafikia hatua za juu

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.