Tuesday, November 21, 2023

BALOZI MBUNDI AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA MKUTANO WA MAKATIBU WAKUU EAC


Katibu Mkuu anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Stephen P. Mbundi ameongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha.

Mkutano huo umepitia na kujadili taarifa iliyowasilishwa na timu ya Wataalamu waliokutana jijini hapo kuanzia tarehe 18 - 20 Novemba 2023. Mkutano wa Makatibu Wakuu unafanyika ikiwa ni maandalizi ya kuelekea kwenye Mkutano wa 44 wa Kawaida wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki unaotarajiwa kufanyika tarehe 22 Novemba 2023.
Katibu Mkuu anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Stephen P. Mbundi akifafanua jambo  kwenye Mkutano wa Makatibu Wakuu wa EAC uliokuwa ukiendelea jijini Arusha
Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia Mkutano wa Makatibu Wakuu wa EAC uliokuwa ukiendelea jijini Arusha
Sehemu ya wajumbe kutoka nchi wanachama wa Jumuiya wakifuatilia Mkutano wa Makatibu Wakuu wa EAC uliokuwa ukiendelea jijini Arusha  
Mkutano wa Makatibu Wakuu wa EAC  ukiendelea
Meza Kuu wakifuatilia Mkutano wa Makatibu Wakuu wa EAC uliokuwa ukiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.