Wednesday, November 15, 2023

“TANZANIA NI SEHEMU SALAMA KWA BIASHARA NA UWEKEZAJI” WAZIRI MAKAMBA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.), amezihakikishia sekta binafsi na za umma nchini Uholanzi kuwa Tanzania ni sehemu salama ya biashara na kuwekeza.

Hayo yameelezwa wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uholanzi lililofanyika jijini The Hague, Uholanzi tarehe 14 Novemba 2023.

Kongamano hilo lililotanguliwa na mkutano wa ndani kati ya sekta za umma na binafsi za nchi hizo, ambapo zilitumia fursa hiyo kujadili kwa kina fursa zilizopo Tanzania pamoja na taratibu nyingine zinazotakiwa kufuatwa na wawekezaji na wafanyabiashara kutoka mataifa mengine.

Kongamano hilo lililokuwa na kauli mbiu isemayo “Ushirikiano sawa kwa Maendeleo Jumuishi na Endelevu” liliandaliwa na kuratibiwa na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini The Hague, Uholanzi kwa kushirikiana na Baraza la Biashara kati ya Uholanzi na Afrika (NABC).

Akifungua kongamano hilo Waziri Makamba pia alieleza kuwa Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka azma ya kutekeleza kwa vitendo dira ya Serikali ya kufanikisha ushindani na uanzishaji wa viwanda kwa maendeleo ya Taifa.

Kongamano likiendelea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akihutubia katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uholanzi lililofanyika jijini The Hague, Uholanzi. Kongamano hilo limeratibiwa na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Baraza la Biashara kati ya Uholanzi na Afrika (NABC)

Picha ya pamoja meza kuu na wawakilishi kutoka sekta za umma za Tanzania na Uholanzi walioshiriki katika kongamano hilo.

Mjumbe wa kongamano kutoka Uholanzi akiwasilisha hoja zake kwa Waziri Makamba ili ziweze kufafanuliwa wakati wa kongamano hilo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akisalimiana na Mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchini Uholanzi waliposhiriki katika kongamano.

Mheshimiwa Waziri Makamba akishuhudia zoezi la kubadilishana Hati za Makubaliano ya Ushirikiano (MoUs) kati ya Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzani (TIC), Bw. Gilead Teri na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Biashara kati ya Uholanzi na Afrika, Bi. Rosmarijn Fens wakati wa kongamano hilo jijini The Hague, Uholanzi.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.