Monday, April 16, 2012

Mhe. Membe aongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa CMAG mjini London




Mhe. Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, akiongea jambo na Mhe. Surujrattan Rambachan (katikati), Waziri wa Mambo ya Nje wa Trinidad and Tobago ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mkutano wa Kikosi Kazi cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Madola (Commonwealth Ministerial Action Group - CMAG), na Mhe. Bob Carr, Waziri wa Mambo ya Nje wa Australia, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CMAG.  Mkutano huo ulifanyika katika Malborough House, mjini London tarehe 16 April, 2012.


Mhe. Membe, ambaye aliongoza Ujumbe wa Tanzania, akiwa katika Chumba cha Mkutano wa CMAG.  Wengineo katika picha ni wajumbe kutoka Tanzania, akiwemo Bi. Dora Msechu (wa pili kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.  Tanzania ni mojawapo ya nchi mwanachama wa CMAG, zikiwemo nchi za Australia, Bangladesh, Canada, Jamaica, Maldives, Sierra Leone, Trinidad and Tobago na Vanuatu.



Mhe. Membe akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Bob Carr, Waziri wa Mambo ya Nje wa Australia, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CMAG.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.