Sunday, April 8, 2012

Mhe. Membe mgeni rasmi Tamasha la Pasaka

View FOTO1.JPG in slide show

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akihutubia umati wa watu uliofika kwenye Tamasha la Pasaka lililofanyika hivi karibuni katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kushoto kwa Mhe. Waziri ni Mke wake Mama Dorcas Membe.


View FOTO2.JPG in slide show

Mhe. Membe (wa pili kutoka kushoto) akiwa na viongozi wa dini waliohudhuria Tamasha la Pasaka. Kutoka kushoto ni Askofu Sylivester Gamanywa wa WAPO Missions akifuatiwa na Mtume Fernandes wa Agape Missions na mwisho ni Mama Membe.
View FOTO3.JPG in slide show

Mhe. Waziri Membe akizindua albamu mpya ya nyimbo za injili iitwayo Kwa Utukufu wa Mungu ya mwimbaji wa nyimbo za injili Solomon Mukubwa kutoka Kenya wakati wa Tamasha la Pasaka.


View FOTO4.JPG in slide show

Mhe. Membe kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wageni waalikwa na waimbaji wa nyimbo za injili waliohudhuria Tamasha la Pasaka.

View FOTO5.JPG in slide show

Mhe. Membe na Mkewe (kulia) wakiwa na Rebecca Malope mwimbaji mashuhuri wa nyimbo za injili kutoka Afrika Kusini wakati wa Tamasha la Pasaka.


View FOTO6.JPG in slide show

Baadhi ya Wabunge na Balozi Liberata Mulamula kwenye Tamasha la Pasaka.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.