Saturday, April 7, 2012

Wizara yamuaga Balozi wa Ireland nchini


View FOTO1.JPG in slide show

Mhe. Balozi Liberatta Mulamula, Msaidizi Mwandamizi wa Rais katika Masuala Diplomasia akitoa hotuba kwa niaba ya Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wakati wa hafla fupi ya chakula cha mchana kilichoandaliwa maalum kwa ajili ya kumuaga Mhe. Lorcan Fullam, Balozi wa Ireland aliyemaliza muda wake wa kazi hapa nchini. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Double Tree.


View FOTO2.JPG in slide show

Balozi  Mulamula akiwa pamoja na Mhe. Fullam wakati wa hafla ya kumuaga Balozi huyo.


View FOTO3.JPG in slide show 
  
Mhe. Lorcan Fullam, Balozi wa Ireland aliyemaliza muda wake wa kazi hapa nchini akizungumza machache wakati wa hafla ya kumuaga.
 
 
View FOTO4.JPG in slide show
 
Balozi Fullam akifurahia zawadi ya Picha ya Wanyama aliyokabidhiwa na Balozi Mulamula kama kumbukumbu ya Tanzania atakapoondoka.
 
 
View FOTO5.JPG in slide show
 
Baadhi ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini na Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa walioshiriki hafla ya kumuaga Balozi Fullam


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.