Thursday, December 18, 2014

BALOZI DORA MSECHU AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO KWA RAIS WA ESTONIA.


Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Dora Msechu amewasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais wa Estonia, Mhe. Toomas Hendrik Ilves.  Balozi Msechu pia alitembelea Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Tallin na kuzungumza, Tea Varrak ambaye ni Rector wa Chuo hicho. Mazungumzo hayo yalilenga kuanzisha ushirikiano kati ya Chuo hicho na vyuo vya vyetu vya UDSM na UDOM na pia kutafuta fursa zaidi za masomo ya sayansi kwa ngazi ya Shahada ya Uzamili (Masters) na Shahada ya Uzamivu (Phd). Estonia ni moja ya nchi iliyopiga hatua kubwa sana katika masuala ya ICT.
Wakiwa chuoni hapo.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.