Monday, December 8, 2014

Waziri Membe akutana na Mabalozi wa Misri na Ufaransa hapa nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akimkaribisha Ofisini kwake Balozi wa Misri hapa nchini Mhe. Hossam Moharam alipofika kwa mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Misri.
Waziri Membe akizungumza na Balozi Moharam.
Mhe. Membe akisalimiana na Balozi wa Ufaransa hapa nchini Mhe. Malika Berak alipofika Ofisini kwake kwa mazungumzo. 

Waziri Membe akizungumza na Balozi Berak huku Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine akisikiliza. Katika mazungumzo yao walisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano katika nyanja mbalimbali ikiwemo kukuza biashara baina ya nchi hizi mbili.




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.