Wednesday, December 3, 2014

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar afanya ziara nchini Comoro

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Seif Sharif Hamad akilakiwa mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Prince Said Ibrahim Hahaya nchini Comoro kwa ziara binafsi uanzia tarehe 1 hadi 4 Desemba, 2014.
Mhe. Hamad akisalimiana na Mhe. Muhammad Ali Soilihi, Makamu wa Rais wa Comoro. Kushoto ni Mhe. Chabaka Kilumanga, Balozi wa Tanzania nchini Comoro na kulia Dkt. Ahamada Albadaoui Fakih, Balozi wa Comoro nchini Tanzania.
Mhe. Hamad akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar, Balozi Silima Haji
Mhe. Hamad akiwa na baadhi ya Masheikh na Viongozi aliofutana nao
================================================



Mhe. Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amefanya ziara binafsi visiwani Comoro kuanzia tarehe 1 hadi tarehe 4 Desemba 2014. Madhumuni ya ziara hii yalikuwa ni kushiriki katika maadhimisho ya miaka arobaini (40) tangu kufariki kwa Marehemu Sheikh Alhabib Omar bin Sumeti, mwanazuoni mashuhuri katika eneo la 
Bahari ya Hindi, ambaye aliwahi kuishi, kujifunza na kutoa elimu Visiwani Zanzibar.

Akiwa nchini Comoro, Mhe. Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar alipata pia fursa ya kuonana na Mhe. Dkt. Ikililou Dhoinine, Rais wa Muungano wa Visiwa vya Comoro, na Mhe. Muhammad Ali Soilihi, Makamu wa Rais wa Comoro. Katika mazungumzo yake na viongozi hao, Mhe. Makamu wa Rais alisifia juhudi zinazochukuliwa kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Comoro. Alibainisha kuwa zipo fursa nyingi za ushirikiano ambazo endapo zitafanyiwa kazi, zitazinufaisha zaidi pande hizi mbili. Aidha, Mhe. Seif Sharif Hamad alikutana na Jumuiya ya Watanzania wanaishi Nchini Comoro na kuzungumza nao.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.