Wednesday, April 6, 2016

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda afanya mazungumzo na Balozi wa Namibia nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Innocent Shiyo akizungumza na Balozi wa Namibia nchini Mhe. Theresia Samaria alipomtembelea leo katika ofisi za Wizara.Katika mazungumzo yao alieleza juu ya umuhimu wa kuimarisha Uhusiano baina ya maitaifa hayo sambamba na kuahidi kuwa Wizara itaendelea kusimamia diplomasia ya Uchumi kama Sera ya Mambo ya Nje inavyoeleza

Mhe. Samaria pia katika mazungumzo hayo alieleza nia ya dhati ya Serikali ya Namibia katika kuimarisha ushirikiano ambapo alieleza umuhimu wa kufanyia utekelezaji makubaliano yanayo sainiwa baina ya mataifa hayo,  hususan katika masuala yanayogusa uchumi, vilevile aliainisha masuala kadhaa ya mafanikio yaliyopatikana katika Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC)
Maafisa Mambo ya Nje katika Wizara ya Mambo ya Nje,Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa wakifuatilia mazungumzo.
Mazungumzo yakiendelea
Wakiagana mara baada ya mazungumzo.

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.