Wednesday, September 6, 2017

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda akutana na Balozi wa India nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Innocent Shiyo akizungumza na Balozi wa India hapa nchini, Mhe.Sandeep Arya alipotembelea Wizarani hivi karibuni. Katika mazungumzo yao Balozi Shiyo alimweleza Balozi Arya masuala mbalimbali kuhusu Tanzania na ushiriki wake katika masuala ya kikanda ikiwemo amani, siasa na usalama hususan katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC)
Mazungumzo yakiendelea kati ya Balozi Shiyo na Balozi Arya. Wengine katika picha ni Afisa kutoka Ubalozi wa India (Kushoto) na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Isaac Isanzu (kulia)
Balozi Shiyo na Balozi Arya katika picha ya pamoja
Balozi Shiyo akiagana na Balozi Arya mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.