Friday, July 20, 2018

Makatibu Wakuu Wizara ya Mambo ya Nje na Wizara ya Habari wakutana kwa kikao kazi

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kushoto) pamoja na mwenyekiti mwenza Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi. Suzan Mlawi wakiongoza kikao kazi cha pamoja baina ya wizara hizo mbili kilichofanyika wizarani jijini Dodoma tarehe 20 Julai 2018.

Wakurugenzi na maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakifuatilia kikao ambacho ni sehemu ya vikao vinavyofanywa na Wizara ya Mambo ya nje katika kuratibu na kufanya ufuatiliaji wa masuala mbalimbali ya kikanda na kimataifa yanayotekelezwa na sekta nyingine nchini.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.