Thursday, April 15, 2021

BALOZI BRIGEDIA JENERALI IBUGE AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI MKOANI MWANZA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge leo ameanza ziara ya kikazi ya siku tatu Mkoani Mwanza. Ziara hii inalenga kufuatilia maendeleo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa na Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria (LVBC) katika Ukanda wa Ziwa Victoria. 

Akiwa mkoani Mwanza Balozi Brigedia Jenerali Ibuge ametembelea mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi katika Bonde la Ziwa Victoria uliopo Walayani Magu, Mwanza. Utekelezaji wa mradi huu wa Kikanda unaratibiwa na Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria chini ya ufadhili na Adaptation Fund (AF). Mradi huu utatekelezwa kwa muda wa miaka mitatu ambapo pia utahusisha Nchi zingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo ni Burundi, Rwanda, Kenya na Uganda.

Balozi Brigedia Jenerali Ibuge akiwa katika eneo la mradi ameeleza kuridhishwa na ubunifu wa mradi huo na kuwaeleza wananchi waliojitokeza kuwa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inafautilia utekelezaji wa mradi huo wa mazingira unaowanufanisha wakazi wa eneo hilo kwa sababu unatekelezwa chini ya Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na hivyo Wizara ndio yenye dhamana ya kuratibu masuala yote yanayohusu au kutokana na Jumuiya. “Hatuwezi tukawa tunaenda kwenye vikao na kuzungumzia kuhusu kutumia pesa za walipa kodi katika kutekeleza miradi bila sisi wenyewe kufika kuona na kujiridhisha juu ya ubora na maendeleo ya miradi husika; Niwahakikishie, haya yote yanafungamana na namna serikali mliyoichagua inavyowajali katika kuleta maendeleo yetu sote kwa pamoja” ameeleza Balozi Brigedia Jenerali Ibuge. 

Mtendaji wa Sekretarieti ya Bonde la Ziwa Victoria Dkt. Ally Said Matano kwa upande wake ameeleza kuwa, LVBC itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kubuni na kutekeleza miradi itakayo tatua changamoto katika jamii na kuchagiza maendeleo ya Nchi na watu wake.

Kabla ya kuanza kwa ziara hiyo Balozi Brigedia Jenerali Ibuge alikutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Mwaza Mhe. John V.K. Mongela na Katibu Mtendaji wa Sekretarieti ya Bonde la Ziwa Victoria Dkt. Ally Said Matano ambaye pia aliambatana naye katika ziara ya kutembelea miradi. Balozi Brigedia Jenerali Ibuge ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanaitunza miradi hiyo na kuitumia ipasavyo ili kuboresha maisha yao kama ilivyokusidiwa kwenye malengo ya kuanzishwa kwake. 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge (kushoto) akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John V.K Mongela.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John V.K Mongela wakiwa katika mazungumzo pamoja na watendaji wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria na Wizara.
Kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii,Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Eliabi Chodota, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John V.K Mongela, Mtendaji wa Sekretarieti ya Bonde la Ziwa Victoria (LVBC) Dkt. Ally Said Matano na Mhandisi Hilda Luoga kutoka LVBC
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akiwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya wa Magu.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Magu Mhe. Salum A. Kalli kwenye ukaguzi wa Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi katika Bonde la Ziwa Victoria uliopo Walayani humo.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akiongea na baadhi ya wananchi wa Magu (hawapo pichani) waliojitokeza kwenye ziara yake ya ukaguzi wa mradi.


 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akielekeza jambo kwa Watendaji alipotembelea eneo la Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi uliopo wilayani Magu, Mwanza.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.