Sunday, April 25, 2021

NAIBU WAZIRI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWENYEKITI WA KAMATI YA SERIKALI YA URUSI

Tarehe 25 Aprili 2021, kwenye Ofisi za Wizara jijini Dar es Salaam, Mheshimiwa Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alikutana na kufanya mazungumzo na Balozi Oleg Ozerov, Mwenyekiti wa Kamati ya Serikali ya Urusi inayosimamia Maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika na Urusi ( Africa- Russia Summit). Mazungumzo hayo yaliyohudhuriwa pia na Mheshimiwa Yuri Popov, Balozi wa Urusi hapa nchini. 

Mbali na majadiliano yaliyolenga kuimarisha na kuendeleza mahusiano baina ya Mataifa haya mawili pia walijadili namna bora ya kufanya Mkutano ujao (Afica-Russia Summit) utakaofanyika 2022 kuwa na tija zaidi kwa Mataifa ya Afrika ikiwemo kuona maeneo ambayo Urusi ingweza kuongeza uwekezaji wake barani Afrika badala ya mfumo wa sasa wa Makampuni ya Urusi kufanya biashara zaidi. Aidha, walibadilishana mawazo kuhusu agenda na mada zinazoweza kujadiliwa katika Mkutano huo wa pili wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika na Urusi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb),  akiagana na Balozi Oleg Ozerov, Mwenyekiti wa Kamati ya Serikali ya Urusi inayosimamia Maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika na Urusi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb),  akiwa katika  mazungumzo na Balozi Oleg Ozerov, Mwenyekiti wa Kamati ya Serikali ya Urusi inayosimamia Maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika na Urusi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.