Tuesday, April 6, 2021

MAPOKEZI YA KATIBU MKUU, NAIBU KATIBU MKUU KATIKA OFISI NDOGO ZA WIZARA - DAR

 Na Mwandishi wetu, Dar

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameendelea kumuamini Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge katika nafasi ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Balozi Ibuge aliteuliwa Februari 06, 2020 kuwa katibu mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki nafasi anayoendelea kuishikilia mpaka sasa.

Kabla ya wadhifa huo, Balozi Ibuge alikuwa Mkuu wa Itifaki (Chief of Protocal) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemuapisha Balozi Fatma Mohammed Rajab kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Balozi Fatma aliteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Qatar Desemba 03, 2016 nafasi aliyokuwa akiishikilia hadi alipoteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (Hayupo Pichani) akimuapisha Balozi Fatma Mohammed Rajab kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo Ikulu Jijini Dar es Salaam



Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo Mhe. Balozi Fatma Mohammed Rajab wakipokelewa na baadhi ya watumishi katika Ofisi Ndogo za Wizara leo Jijini Dar es Salaam


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo Mhe. Balozi Fatma Mohammed Rajab mara baada ya kuwasili katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Fatma Mohammed Rajab akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Wizara wakati wa mapokezi katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam 


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Fatma Mohammed Rajab akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam 



  

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.