Tuesday, December 15, 2015

Balozi Mulamula afungua Mkutano wa Asasi za Kiraia wa Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akizungumza wakati akifungua rasmi Mkutano wa siku mbili wa Asasi za Kiraia kutoka Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu uliofanyika katika Hoteli ya Golden Tulip Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo uliwashirikisha wenyeviti wa asasi za kiraia kutoka nchi wanachama wa Ukanda wa Maziwa Makuu.
Sehemu ya Wajumbe wakifuatilia ufunguzi wakati Katibu Mkuu, Balozi Mulamula akizungumza (hayupo pichani)
Sehemu nyingine ya wajumbe wakifuatilia ufunguzi
Wajumbe wengine wa mkutano
Mwenyekiti wa Asasi za Kiraia eneo la Maziwa  Makuu ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mzee Joseph Butiku akizungumza wakati wa mkutano huo.  

Wajumbe wakifuatilia wakati Mzee Butiku akizungumza
Balozi Mulamula akiagana na Mzee Butiku mara baada y akufungua mkutano
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Samwel Shelukindo (kushoto) akizungumza na mmoja wa washiriki wa mkutano mara baada ya ufunguzi

Balozi Mulamula akizungumza na Wandishi wa Habari kuhusu umuhimu wa Asasi za Kiraia katika eneo la Maziwa Makuu.
Picha ya Pamoja kati ya mgeni rasmi Balozi Mulamula na Wajumbe wa Mkutano

=================================

BALOZI MULAMULA: ASASI ZA KIRAIA ZINA MCHANGO MKUBWA KATIKA AMANI UKANDA WA MAZIWA MAKUU

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula  amesema kuwa Asasi za Kiraia zina nafasi kubwa katika utatuzi wa migogoro na kuleta amani hususan katika eneo la Ukanda wa Maziwa Makuu na Afrika kwa ujumla.

Balozi Mulamula aliyasema hayo jana wakati akifungua mkutano wa Wenyeviti wa Asasi za Kiraia kutoka Nchi za Maziwa Makuu unaofanyika kwa siku mbili katika Hoteli ya Golden Tulip, Jijini Dar es Salaam.

Balozi Mulamula ambaye pia aliwahi kuwa Katibu Mtendaji wa Kwanza wa Sekretarieti ya Maziwa Makuu alisema kuwa kwa uzoefu wake utatuzi wa migogoro, kulinda amani na katika kuhakikisha demokrasia na utawala wa sheria vinafuatwa kila chombo kina nafasi na umuhimu wake  na kwamba Asasi za Kiraia zina nafasi kubwa zaidi kwani zinawakilisha maoni ya wananchi.

“Asasi za Kiraia ni chombo muhimu sana katika kuhakikisha amani inakuwepo hususan katika Ukanda wa Maziwa Makuu kwani zinawawakilisha wananchi moja kwa moja hivyo ni vizuri kutambua nafasi yenu”, alisema Balozi Mulamula.

Aidha, aliipongeza Asasi hiyo ya ambayo kwa kiasi kikubwa imefanikiwa tangu ilipoanzishwa mwaka 2011 na kusisitiza ijikite zaidi katika kutekeleza  majukumu yake ikiwa ni pamoja na kuhakikisha misingi ya demokrasia, utawala bora na utawala wa sheria katika nchi za Ukanda wa Maziwa makuu vinafuatwa na kutekelezwa kikamilifu.

“Najua mnazijua hadidu za rejea na wajibu wenu kama Asasi  za Kiraia, ni kuhakikisha nchi wanachama zinafuata misingi ya sheria, utawala bora na ule wa sheria ili kuepuka migogoro ya mara kwa mara katika eneo letu la Maziwa Makuu”, alisisitiza Balozi Mulamula.

Awali akimkaribisha Balozi Mulamula kuzungumza, Mwneyekiti wa Mkutano huo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mzee Joseph Butiku alisema kwamba mkutano huo wa Wenyeviti wa Asasi kutoka nchi wanachama wa Maziwa Makuu ni muhimu sana hususan katika kipindi hiki ambapo pamoja na mambo mengine utaandaa na kupitisha agenda za Asasi hiyo zitakazowasilishwa kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi unaotarajiwa kufanyika mwezi Februari, 2016.

Aidha, aliongeza kuwa wakati umefika kwa Nchi Wanachama wa Maziwa Makuu kutambua mchango wa asasi za kiraia  na kuzishirikisha ipasavyo katika msuala muhimu hususan yale ya utatuzi wa migogoro ili kuleta tija kwenye eneo hili la Maziwa Makuu ambalo kwa kiasi kikubwa limekuwa na migogoro ya kisiasa na kikabila.

Mkutano huo wa siku mbili uliwashirikisha Wenyeviti wa Asasi kutoka nchi zote 12 wanachama wa Ukanda wa Maziwa Makuu ikiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, Sudan Kusini, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Jamhuri ya Afrika ya Kati, Rwanda, Jamhuri ya Congo, Angola, Sudan na Zambia.

(Mwisho)

Katibu Mkuu, Balozi Mulamula akutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi wa Shirika la IDLO

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa,  Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Sheria (IDLO) nchini Kenya, Bi. Enid Muthoni. Mkurugenzi huyo alikuja kwa lengo la kulitambulisha shirika hilo ambalo linajishughulisha na kuzijengea uwezo nchi katika masuala ya Utawala wa Sheria. Shirika hilo ambalo  lilianzishwa mwaka 1988  lina Makao Makuu  Mjini Roma, Italia.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Baraka Luvanda. Kulia ni Bw. Abdallah Mtibora, Afisa Mambo ya Nje.
Bi. Muthoni akifafanua jambo kwa Balozi Mulamula kuhusu shirika hilo la IDLO.
Mwakilishi wa IDLO hapa nchini, Prof. Gaston Kennedy kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam nae akitoa maelezo ya nyongeza kuhusu shirika hilo.
Picha ya pamoja

Balozi Mulamula azungumza na Balozi wa Ufaransa nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kulia) akizungumza na Balozi wa Ufaransa hapa nchini, Mhe. Malika Berak.  Katika mazungumzo yao walisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Ufaransa katika sekta mbalimbali ikiwemo uchumi, elimu na jamii kwa ujumla. Mazungumzo hayo yalifanyika Ofisini kwa Balozi Mulamula tarehe 15 Desemba, 2015.
Maafisa kutoka Wizarani na Ubalozi wa Ufaransa wakimsikiliza Balozi Mulamula (hayupo pichani). Kushoto ni Bi. Felister Rugambwa.
Balozi Mulamula akimsikiliza Balozi Malika wakati wa mazungumzao yao.
Mazungumzo yakiendelea
Balozi Malika akimweleza jambo Balozi Mulamula  wakati wakiagana mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.


Balozi Dkt. Mahiga akutana na Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na iliyokuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula aliyesimama akitoa neno kabla ya kumkaribisha, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga   (katikati) kuongea na Wakuu wa Idara/Vitengo wa Wizara hiyo. Kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba     
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki (wa kwanza kushoto), Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi, Bw. Wilfred Masanja (wa kwanza kulia), na Kaimu Mkuu wa Idara ya Sera na Mipango, Bw. John Ngowo wakisikiliza kwa makini neno la ukaribisho kutoka kwa  Balozi Mulamula akimkaribisha Mhe. Waziri kuzungumza na Wakuu wa Idara/Vitengo.
Sehemu nyingine ya Wakurugenzi walioudhuria kikao hicho, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Negel Msangi, Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, Balozi Anisa Mbega (katikati) na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Balozi Innocent Shiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (wa kwanza kulia), Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Itifaki Bi. Grace Martine (wa kwanza kushoto), Kaimu Mkurugenzi Idara ya Amerika na Ulaya, Bi. Tunsume Mwangolombe (wa pili kutoka kulia) na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Eva Ng'itu nao wakiwa kwenye mkutano wa Mhe. Waziri Mahiga na Mhe. Naibu Waziri Dkt. Kolimba (hwapo pichani).
Sehemu nyingine ya Viongozi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Samuel Shelukindo, Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani Bw. Marthias Abisai (wa kwanza kushoto), na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA Bw. Nassoro Msumi (katikati).  
Kikao kikiendele


========Kikao na Uongozi wa iliyokuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki========
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (wa pili kutoka kushoto), na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Suzani Kolimba (wa kwanza kushoto) wakimsiliza kwa makini Katibu Mkuu wa Iliyokuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Joyce Mapunjo (wa pili kutoka kulia) katika kikao baina ya Mhe. Waziri na Wakuu wa Idara na Vitengo, wa iliyokuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Mwingine katika picha ni Naibu Katibu Mkuu, Bw. Amantius Msole.
Mhe. Joyce Mapunjo akiwatambulisha Wakurugenzi wake (hawapo pichani) kwa Mhe. Waziri Mahiga na Naibu Waziri Kolimba
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ulinzi na Siasa Bw. Amani Mwatonoka akijitambulisha kwa Mhe. Waziri Mahiga na Naibu Waziri Dkt. Kolimba (hawapo pichani).
Wakurugenzi na Wakurugenzi Wasaidizi wakifuatilia kwa makini kikao kilichokuwa kinaendelea.
Makatibu wa Mawaziri nao wakifuatilia kwa makini mkutano huo, wa kwanza kushoto ni Bw. Thobias Makoba, na Adam Isara (wa kwanza kulia).
Kikao kikiendelea
Picha na Reginald Philip


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Naibu Waziri wake, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba waliwasili Wizarani kuanza kazi rasmi siku ya Jumamosi tarehe 12 Desemba 2015. Viongozi hao wapya wa Wizara walipokelewa na watumishi kwa shangwe walipowasili wizarani, muda mfupi baada ya kula kiapo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika Ikulu ya Dar es Salaam.  

Siku ya kwanza Wizarani, Waheshimiwa Mawaziri walipata fursa ya kukutana na uongozi wa Wizara ukiongozwa na Katibu Mkuu, Balozi Liberata Mulamula na Katibu Mkuu wa iliyokuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Joyce Mapunjo. Makatibu Wakuu hao pamoja na mambo mengine, walikabidhi kwa Waheshimiwa Mawaziri nyaraka muhimu za Wizara zitakazowaongoza katika utekelezaji wa majukumu yao.


Aidha, walitumia fursa hiyo kueleza utekelezaji wa majukumu ya Wizara na masuala ambayo yanahitaji miongozo yao ili yaweze kufanyiwa kazi na kukamilishwa.

Balozi Mahiga na Dkt. Kolimba walipata fursa pia ya kutembelea watumishi wa iliyokuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki siku ya tarehe 14 Desemba 2015 kwenye Jengo la Waterfront. Watumishi hao kama walivyofanya wenzao waliwapokea viongozi wapya kwa shangwe na baadaye kufanya kikao na Wakuu wa Idara na Vitengo.


Katika vikao vyote,  Mhe. Waziri aliomba ushirikiano kutoka kwa Wakuu wa Idara/Vitengo na watumishi wote kwa jumla ili kwa pamoja waweze kuendana na kasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye kaulimbiu ya “Hapa kazi tu”




Saturday, December 12, 2015

Waziri na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wakaribishwa rasmi katika Ofisi zao tayari kuanza kazi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Augustine Mahiga akisaini Kitabu cha Wageni alipowasili Ofisini kwake kwa mara ya kwanza baada ya kuapishwa. 
Mhe. Balozi Mahiga akifurahia jambo Ofisini kwake na Makatibu Wakuu wa Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa,  Balozi Liberata Mulamula (kushoto) na Bibi Joyce Mapunjo (kulia).
Balozi Mulamula akimkabidhi Mhe. Waziri machapisho mbalimbali ya Wizara ikiwemo Sera ya Mambo ya Nje
Bibi Mapunjo akimkabidhi Mhe. waziri makabrasha mbalimbali ya iliyokuwa Wizara ya Afrika Mashariki
Mhe. Balozi Mahiga akipata picha ya pamoja na Watumishi walio katika Ofisi yake. Kutoka kulia ni Bi. Catherine Kijuu, Katibu Mahsusi wa Waziri, Bw. Thobias Makoba, Katibu wa Waziri na Bi. Nsia Paul, Katibu Mahsusi wa Waziri.
Balozi Mulamula wakati akimwongoza Mhe. Balozi Mahiga kuingia Ofisini kwake kwa mara ya kwanza

.....Naibu Waziri akiwa Ofisini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba akisaini Kitabu cha Wageni alipowasili Ofisini kwake kwa mara ya kwanza baada ya kuapishwa. 
Balozi Mulamula akimkabidhi Mhe. Naibu Waziri machapisho mbalimbali ya Wizara ikiwemo Sera ya Mambo ya Nje
Mhe. Dkt. Kolimba akisaini Kitabu cha Wageni alipowasili Ofisini kwake kwa mara ya kwanza
Mhe. Dkt. Kolimba akiwa katika picha ya pamoja na Katibu wake, Bw. Adam Isara
Mhe. Dkt. Kolimba akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Wizara katika Ofisi yake. Kushoto ni Bi. Eva Mnembuka na Bi. Moshi Ibrahim (kulia)

Picha na Reginald Philip




Waziri na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wawasili rasmi Wizarani baada ya kuapishwa


Waziri wa Mambo wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Balozi Augustine Mahiga akila kiapo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
Naibu Waziri wa Mambo wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Suzani Kolimba akila kiapo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akimkaribisha  Wizarani kwa mara ya kwanza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Augustine Mahiga mara alipowasili Wizarani baada ya kuapishwa Ikulu tarehe 12 Desemba, 2015. Aliyesimama pembeni ni Katibu Mkuu wa iliyokuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bibi Joyce Mapunjo.
Mhe. Balozi Mahiga akikaribishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Simba Yahya.
Mhe. Balozi Mahiga akipokea shada la maua kutoka kwa mmoja wa Watumishi wa Wizara Bi. Nsia Paul wakati wa mapokezi yake Wizarani
Naibu Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Suzan Kolimba akipokea shada la maua kutoka kwa mmoja wa Watumishi wa Wizara Bi. Tagie Mwakawago mara baada ya kuwasili rasmi Wizarani
Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa wakimpokea Mhe. Waziri Wizarani. Pichani Mhe. Waziri akisalimiana na Balozi Anisa Mbega, Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora.
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa wakimkaribisha kwa shangwe na furaha Mhe. Balozi Mahiga Wizarani.
Mhe. Waziri akisalimiana na Watumishi wa Wizara waliojitokeza kumpokea mara baada ya kuwasili Wizarani rasmi baada ya kuapishwa.
Katibu Mkuu wa iliyokuwa Wizara Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bibi Mapunjo akijitambulisha rasmi kwa Waziri, Mhe. Balozi Mahiga na Mhe. Naibu Waziri, Mhe. Kolimba (kushoto).
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Simba Yahya akijitambulisha  rasmi kwa Waziri, Mhe. Balozi Mahiga na Mhe. Naibu Waziri, Mhe. Kolimba (kushoto). Mwingine katika picha ni Katibu Mkuu, Balozi Mulamula
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa akiongea jambo wakati wa mapokezi ya Mhe. Waziri na Naibu Waziri.
Waziri, Mhe. Balozi Mahiga kwa pamoja na Naibu Waziri, Mhe. Kolimba wakiwa katika picha ya pamoja na Makatibu Wakuu, Balozi Mulamula na Bibi Mapunjo na Naibu Makatibu Wakuu, Balozi Yahya na Bw. Amantius Msole (wa kwanza kulia)
Picha ya pamoja

Picha na Reginald Philip