Tuesday, December 15, 2015

Balozi Mulamula azungumza na Balozi wa Ufaransa nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kulia) akizungumza na Balozi wa Ufaransa hapa nchini, Mhe. Malika Berak.  Katika mazungumzo yao walisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Ufaransa katika sekta mbalimbali ikiwemo uchumi, elimu na jamii kwa ujumla. Mazungumzo hayo yalifanyika Ofisini kwa Balozi Mulamula tarehe 15 Desemba, 2015.
Maafisa kutoka Wizarani na Ubalozi wa Ufaransa wakimsikiliza Balozi Mulamula (hayupo pichani). Kushoto ni Bi. Felister Rugambwa.
Balozi Mulamula akimsikiliza Balozi Malika wakati wa mazungumzao yao.
Mazungumzo yakiendelea
Balozi Malika akimweleza jambo Balozi Mulamula  wakati wakiagana mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.