Wednesday, December 16, 2015

Waziri Mahiga afanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC na Balozi wa Marekani nchini

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akimkaribisha Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Dkt. Stergomena Tax alipofika Wizarani kwa ajili ya kumpongeza kwa kuteuliwa katika wadhifa huo na pia kumpatia taarifa fupi kuhusu muundo, majukumu na utendandaji wa Jumuiya ya SADC.Mazungumzo hayo yalifanyika Wizarani Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Desemba, 2015.
Mhe. Dkt. Mahiga akimweleza jambo Dkt. Tax wakati wa mazungumzo yao.
Wajumbe waliofutana na Mhe. Dkt. Tax wakinukuu mazungumzo ya viongozi hao ambao hawaonekani pichani.
Mhe. Dkt. Tax akifafanua jambo kwa Mhe. Dkt. Mahiga.
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Balozi Innocent Shiyo akiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga pamoja na Bw. Thobias Makoba, Msaidizi wa Waziri.
Mazungumzo yakiendelea

..........Mkutano na Balozi wa Marekani

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akimkaribisha  Balozi wa Marekani hapa nchini, Mhe. Mark Childress alipofika Wizarani kwa lengo la kumpongeza  kwa kuteuliwa na Mhe. Rais kwenye wadhifa huo na pia kuzungumzia masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na Marekani.
Mhe. Dkt. Mahiga akizungumza na Balozi Childress ambapo alimhakikishia ushirikiano Balozi huyo.
Balozi Childress nae akizungumza.
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Balozi Joseph Sokoine akiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali pamoja na Msaidizi wa Waziri, Bw. Thobias Makoba nao wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Dkt. Mahiga na Balozi Childress (hawapo pichani).
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo
Mazungumzo yakiendelea
Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.