Monday, December 21, 2015

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Mabalozi Wateule wa Korea na EU nchini

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirkiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Jamhuri ya Korea nchini, Mhe. Song Geum-young. Tukio hilo lilifanyika Wizarani tarehe 21 Desemba, 2015.
Mhe. Dkt. Mahiga akiwa kwenye mazungumzo na Balozi Song Geum-young mara baada ya kupokea nakala za hati za utambulisho.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto) akiwa na Bw. Thobias Makoba (kulia), Msaidizi wa Waziri  pamoja na Bw. Khatib Makenga (katikati), Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo kati ya Dkt. Mahiga na Balozi Song Geum-young (hawapo pichani)
Kaimu Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bw. James Bwana akimpatia utaratibu  Balozi Song Geum-young kabla ya kuwasilisha Nakala zake za Utambulisho kwa Mhe. Waziri

 .......Nakala za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa EU

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirkiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akimkaribisha  Balozi Mteule wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Mhe. Roeland Van De Geer alipofika Wizarani kwa ajili ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Mhe. Waziri. Tukio hilo lilifanyika Wizarani tarehe 21 Desemba, 2015.
Mhe. Dkt. Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa  Balozi Mteule wa Umoja wa Ulaya hapa nchini, Mhe. Roeland Van De Geer.
Mhe. Dkt. Mahiga akizungumza na Balozi Mteule wa EU, Mhe. Roeland Van De Geer
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirkiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine akiwa na Bi. Felister Rugambwa wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Dkt. Mahiga na Balozi Roeland Van De Geer  (hawapo pichani)

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.