Tuesday, December 22, 2015

Waziri Mahiga akutana kwa mazungumzo na Balozi wa China nchini

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akimkaribisha Balozi wa China hapa nchini, Mhe. Dkt. Lu Youqing  alipofika Wizarani kwa ajili ya kumpongeza kwa kuteuliwa katika wadhifa huo mpya na pia kuzungumzia masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na China. Pembeni ni Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki.
Balozi Lu Youqing akizungumza na Mhe. Dkt. Mahiga kuhusu mwenendo wa ushirikiano kati ya Tanzania na China ikiwemo miradi mbalimbali ya maendeleo inayofanywa nchini kwa ushirikiano na China.
Balozi Mbelwa na Bw. Thobias Makoba, Msaidizi wa Waziri wakifuatilia mazungungumzo kati ya Mhe. Dkt. Mahiga na Balozi Lu (hawapo pichani)
Sehemu ya ujumbe kutoka Ubalozi wa China wakifuatilia mazungumzo
Mazungumzo yakiendelea
Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.