Friday, December 4, 2015

Ujenzi wa Mahakama ya Kimataifa waanza jijini Arusha.



Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Baraka Luvanda (wa pili kulia), Msajili wa MICT Bw. John Hocking (wa pili kushoto) Afisa wa MICT Bw. Bw. Samwel Akorimo (wa kwanza kulia) na Afisa Mambo ya Nje Bw. Elisha Suku (wa kwanza kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja. 

Umoja wa Mataifa umeanzisha mradi wa ujenzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Masalia ya kesi za Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (Mechanism for International Criminal Tribunals (MICT) katika eneo la Lakilaki jijini Arusha.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Baraka Luvanda, kwa niaba ya Wizara hiyo ametembelea mradi huo tarehe 02/12/2015 ili kujionea maendeleo ya ujenzi huo.

Ujenzi huo unahusisha masijala ya nyaraka mbalimbali za Mahakama ya kimataifa ya mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) ambayo inahitimisha shughuli zake tarehe 31/12/2015.

Eneo hilo la Lakilaki limetengwa mahsusi kwaajili ya taasisi mbalimbali za kimataifa ambapo mpaka sasa taasisi kama United Nations for International Criminal Tribunal (UNMICT), African Union Advisory Board on Corruption (AUABC), African Institute of International Law (AIIL) na African Court on Human and Peoples' Rights (ACHPR) zinatarajiwa kuwa na ofisi katika jengo hilo.

Pamoja na ziara hiyo, Balozi Luvanda alipata fursa ya kushiriki kwenye uzinduzi wa mnara wa amani (The Arusha Peace Park Monument), tarehe 30/12/2015 mnara ambao  umejengwa  na ICTR kama kumbukumbu ya kudumu kufuatia kuhitimisha shughuli zake jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.