Tuesday, December 15, 2015

Katibu Mkuu, Balozi Mulamula akutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi wa Shirika la IDLO

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa,  Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Sheria (IDLO) nchini Kenya, Bi. Enid Muthoni. Mkurugenzi huyo alikuja kwa lengo la kulitambulisha shirika hilo ambalo linajishughulisha na kuzijengea uwezo nchi katika masuala ya Utawala wa Sheria. Shirika hilo ambalo  lilianzishwa mwaka 1988  lina Makao Makuu  Mjini Roma, Italia.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Baraka Luvanda. Kulia ni Bw. Abdallah Mtibora, Afisa Mambo ya Nje.
Bi. Muthoni akifafanua jambo kwa Balozi Mulamula kuhusu shirika hilo la IDLO.
Mwakilishi wa IDLO hapa nchini, Prof. Gaston Kennedy kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam nae akitoa maelezo ya nyongeza kuhusu shirika hilo.
Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.