Tuesday, December 1, 2015

Balozi wa Afrika Kusini nchini amtembelea Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Afrika Kusini hapa nchini Mhe. Thamsanga Dennis Mseleku katika mazungumzo yaliyolenga kuboresha mahusiano mema na ya muda mrefu baina ya nchi hizo mbili.  
Balozi Thamsanga Dennis Mseleku, akisisitiza jambo kwa Katibu Mkuu Balozi Mulamula.
Mazungumzo yakiendelea huku Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto), Bw. Merdard Ngaiza, Afisa Mambo ya Nje (katikati) pamoja na Afisa Habari wa Mambo ya Nje, Bw. Ally Kondo wakifuatilia mazungumzo hayo.
    
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula akiagana na Balozi wa    Afrika Kusini hapa nchini Mhe. Thamsanga Dennis Mseleku,           baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Wizarani tarehe 01/12/2015.
                         =========================
                           Picha na Reuben Mchome.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.