Wednesday, December 23, 2015

Waziri Mahiga akutana kwa mazungumzo na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa waliopo nchini

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na  Kimataifa, Dkt. Augustine Mahiga akizungumza kwa mara ya kwanza kwenye mkutano uliomkutanisha na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa yaliyopo hapa nchini. Mkutano huo ulikuwa na lengo la Waziri kujitambulisha ambapo pia alitoa taarifa mbalimbali ikiwemo umuhimu wa ushirikiano wa Tanzania na nchini mbalimbali; hali ya kisiasa huko Zanzibar baada ya uchaguzi na mgogoro wa kisiasa unaoendelea nchini Burundi.
Sehemu ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakimsikiliza kwa makini Balozi Mahiga (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao, wa kwanza kushoto ni Balozi wa Rwanda nchini, Mhe. Eugene Segore Kayihura (wa kwanza kushoto), Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Mark Children (wa pili kutoka kushoto), Balozi wa Oman nchini Mhe. Soud Al Mohammed Al-Ruqaish
Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini nao wakimsikiliza kwa makini Waziri Mahiga (hayupo pichani)
Sehemu nyingine ya Mabalozi na Makaimu Balozi waliohudhuria mkutano huo. Balozi wa China nchini Mhe. Lu Youqing (wa pili kutoka kulia kwenye mstari wa pili), Naibu Balozi wa Misri, Bw. Moataz Kareem Elbahnasawi (wa kwanza kulia mstari wa mbele).
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Dkt. Suzan Kolimba naye alipata fursa ya kujitambulisha kwa Mabalozi na Wakuu hao wa Mashirika.
Sehemu nyingine ya Mabalozi wakimsikiliza Naibu Waziri Kolimba (hayupo pichani) alipokuwa akijitambulisha kwao. 
Katibu Mkuu wa iliyokuwa Wizara ya Afrika Mashariki, Mhe. Joyce Mapunjo na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika nao wakimsikiliza kwa makini Waziri Mahiga (hayupo pichani). 
Sehemu ya Wakurugenzi wa iliyokuwa Wizara ya Afrika Mashariki 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Bi. Amisa Mwakawago na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Bw. Abdallah Mtibora
Waziri Mahiga akiendelea kuzungumza
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Bi. Mindi Kasiga akizungumza
Sehemu ya Wakurugenzi na Wakurugenzi Wasaidizi kutoka iliyokuwa Wizara ya Afrika Mashariki
Waziri Mahiga akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya  mazungumzo na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa, na Wakuu wa Mashariki ya Kimataifa nchini.
Waziri Mahiga (kushoto) akisalimiana na Naibu Balozi wa Misri, Bw. Moataz Kareem Elbahnasawi (katikati) na kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Itifaki, Bw. James Bwana
Naibu Waziri akisalimiana na Balozi wa Demokrasia ya Kongo Mhe.Halfan Juma Mpango
Waziri Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa nchini 

Picha ya pamoja



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.