Saturday, December 12, 2015

Waziri na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wakaribishwa rasmi katika Ofisi zao tayari kuanza kazi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Augustine Mahiga akisaini Kitabu cha Wageni alipowasili Ofisini kwake kwa mara ya kwanza baada ya kuapishwa. 
Mhe. Balozi Mahiga akifurahia jambo Ofisini kwake na Makatibu Wakuu wa Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa,  Balozi Liberata Mulamula (kushoto) na Bibi Joyce Mapunjo (kulia).
Balozi Mulamula akimkabidhi Mhe. Waziri machapisho mbalimbali ya Wizara ikiwemo Sera ya Mambo ya Nje
Bibi Mapunjo akimkabidhi Mhe. waziri makabrasha mbalimbali ya iliyokuwa Wizara ya Afrika Mashariki
Mhe. Balozi Mahiga akipata picha ya pamoja na Watumishi walio katika Ofisi yake. Kutoka kulia ni Bi. Catherine Kijuu, Katibu Mahsusi wa Waziri, Bw. Thobias Makoba, Katibu wa Waziri na Bi. Nsia Paul, Katibu Mahsusi wa Waziri.
Balozi Mulamula wakati akimwongoza Mhe. Balozi Mahiga kuingia Ofisini kwake kwa mara ya kwanza

.....Naibu Waziri akiwa Ofisini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba akisaini Kitabu cha Wageni alipowasili Ofisini kwake kwa mara ya kwanza baada ya kuapishwa. 
Balozi Mulamula akimkabidhi Mhe. Naibu Waziri machapisho mbalimbali ya Wizara ikiwemo Sera ya Mambo ya Nje
Mhe. Dkt. Kolimba akisaini Kitabu cha Wageni alipowasili Ofisini kwake kwa mara ya kwanza
Mhe. Dkt. Kolimba akiwa katika picha ya pamoja na Katibu wake, Bw. Adam Isara
Mhe. Dkt. Kolimba akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Wizara katika Ofisi yake. Kushoto ni Bi. Eva Mnembuka na Bi. Moshi Ibrahim (kulia)

Picha na Reginald Philip




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.