Thursday, June 16, 2016

Katibu Mkuu Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akutana na Balozi wa Sweden nchini


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini Mhe. Balozi Katarina Rangnitt alipomtembelea  Wizarani, Juni 13, 2016.

 Balozi Dkt. Aziz Mlima na Mhe. Katarina Rangnitt wakiwasikiliza Mkurugenzi Mkazi wa TMEA (Trade Mark East Africa) Dkt. Josaphat Kweka ( wa kwanza kushoto kwa Balozi), Bi Sara Spant kutoka  Ubalozi wa Sweden na Bw. Ulf Ekdahl kutoka  Shirika la Maendeleo la Sweden (SIDA) katika Mkutano uliofanyika Wizarani Juni 13,2016

Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz Mlima na Mhe. Balozi Katarina Rangnit wakijadiliana jambo kwenye Mkutano uliofanyika Juni 13, 2016, Wizarani, wanaofuatilia kulia ni  Wakurugenzi  kutoka Wizarani Bw. Geoffrey Mwambe, Bw. Oswald Kyamani na Bw. Eliabi Chodota.

Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz Mlima, Mhe. Balozi Katarina Rangnit , Mkurugenzi  Mkazi wa TMEA, Maafisa wa Ubalozi wa Sweden na  Wakurugenzi kutoka Wizarani katika picha ya pamoja baada ya Mkutano June 13,2016

Dkt. Possi asisitiza umuhimu wa vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu

Mhe. Dkt. Abdallah Possi, (Mb) Naibu Waziri, Ofisi  ya Waziri Mkuu akichangia  majadiliano kuhusu  mada ya  kuwaondololea umaskini na   kukosekana kwa usawa kwa  watu wenye ulemavu. Mhe. Possi alikuwa mmoja wa wanajopo watano walioanzisha majadiliano kuhusu mada hiyo katika siku ya pili ya  Mkutano  wa Tisa wa Mkataba wa Watu  wenye Ulemavu unaoendelea hapa  Umoja wa Mataifa.
Naibu Waziri Possi  akibadilishana   mawazo na   Bi. Asa Regner Waziri wa Watoto, Wazee na Usawa wa Jinsia  kutoka Sweden muda mfupi  kabla ya kuanza kwa majadiliano kuhusu kuwaondolea umaskini na kukosekana kwa usawa kwa watu wenye ulemavu.
Ujumbe wa Tanzania ambao umeongoza na  Mhe, Naibu  Waziri katika  mkutano wa Tisa  wa  Mkataba kuhusu Watu wenye  Ulemavu.  kati ya wajumbe  hao ni,   kutoka kushoto mstari wa nyuma ni  Bi. Ngusekela Karen Nyerere ( Mambo ya Nje) Mhe. Stella Ikupa Alec ( Mb, CCM), Mhe. Riziki Said Lulinda( Mb,CUF) na Mhe. Dkt. Elly Marko Macha( Mb. CHADEMA)  aliyekaa mbele ni  Bi Josephine Makunzo Lyengi, Kaimu Kamishna kuhusu Watu wenye Ulemavu

Wednesday, June 15, 2016

Naibu Waziri Dkt. Possi ashiriki Mkutano wa Tisa wa nchi Wanachama wa Mkataba wa watu wenye Ulemavu


 Naibu Waziri, Ofisi  ya  Waziri Mkuu,(Masuala ya Walemavu)  Mhe. Dr. Abdallah Possi ( Mb) akizungumza wakati wa majadiliano ya jumla kuhusu  utekelezaji wa Mkataba wa Haki za Watu wenye Ulemavu. Mhe. Possi anaongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tisa  wa Nchi  Wanachama  wa Mkataba  wa Watu  Wenye Ulemavu. Mkutano huu wa siku tatu umeanza siku ya  Jumanne hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.  Wajumbe wengine katika  picha ni kutoka kushoto Mhe. Stella Ikupa Alex ( Mb), Mhe. Riziki Said Lulida ( Mb) na Mhe. Elly Marko Macha ( MB). 
Ujumbe wa Tanzania wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa  Tisa wa Mkataba wa Watu  Wenye  Ulemavu,  ufunguzi wa mkutano  huu  ulifanyika katika  Ukumbi Mkuu wa Mikutano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Mkutano huu wa siku tatu ajenda yake ni "Utekelezaji wa  Agenda  ya Maendeleo Endelevu ( Agenda 2030) Kwa Watu Wote Wenye Ulemavu: Pasipo Kumwacha Yeyote”. Unahudhuriwa na  Washiriki kutoka nchi 164   ambazo zimeridhia  Mkataba huu, Asasi zisizo za kiserikali pia  zinahudhuria katika  Mkutano  huu ambao ni  maalum kwa watu wenye ulemavu wa aina zote.

============================================

FURSA ZA KIUCHUMI  NI CHANGAMOTO KUBWA KWA  WATU WENYE ULEMAVU-MHE-POSSI

Mkutanowa Tisa wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu ( CRDP), umeanza  Jumanne)  hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa,  New York, Marekani.

Mada au  ujumbe wa Mkutano huu wa siku tatu ni “ Utekelezajiwa  Agenda  yaMaendeleoEndelevu (Agenda 2030) Kwa Watu Wote Wenye Ulemavu: Pasipo Kumwacha Yeyote”

Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania katika Mkutano huu, unaongozwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Dr. Abdallah Possi( Mb). Wajumbe wengine ni Mhe. Riziki Lulinda (Mb), Mhe. Elly Macha (Mb), Mhe. Stella Ikupa (Mb) , Bi Josephine Lyengi, Kaimu Kamishna kuhusu watu wenye ulemavu na Bi. NgusekelaNyerere , Afisa Mambo yaNje, Wizara ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Akizugumza wakati wa majadiliano ya jumla mara baada ya hafla ya ufunguzi, Naibu Waziri. Dr. Abdallah Possi amesema, changamoto kubwa inayowakabili watu wenye ulemavu nchini Tanzania,  ni fursa za kiuchumi.
“Licha ya mafanikio kadhaa yakiwamo ya utungaji wa sera,  sheria na mabadiliko mbalimbali kuhusu watu wenye ulemavu, bado kuna changamoto nyingi ambazo zinatakiwa kufanyiwa kazi kwa lengo la kuwapunguzia matatizo watu wenye ulemavu yakiwamo matatizo ya kutokuwa na fursa  sawa na kuondokana na umaskini”. Alieleza Naibu  Waziri

Na Kuongeza kwamba, Tanzania kama ilivyo kwa nchi nyingine inakabiliwa pia na vipaumbele vinavyokinzana na ambavyo ni muhimu lakini vikiwaathiri zaidi watu wenye ulemavu.

Akavitaja baadhi ya vipaumbele hivyo kuwa ni pamoja na upatikanaji wa maji safi nasalama, chakula, huduma za afya, elimu na ukosefu wa ajira.

Vile vile Naibu Waziri ameleza kuwa mtazamo hasi kuhusu watu wenye ulemavu ni changamoto nyingine ambayo inatatiza ujumuishi wa watu wenye ulemavu katika fursa mbalimbali za maendeleo ya kiuchumi na kijamii ambazo wangeweza kunufaika nazo bila ya kujali hali zao.

Akizungumzia kuhusu mahitaji ya watu wenye ulemavu nchini Tanzania,  Mhe. Dr. Possi, ameeleza washiriki wa mkutano huu kutoka nchi 164 ambazo zimeridhia mkataba wa watu wenye ulemavu kwamba,  watu wenye ulemavu nchini  Tanzania wanakabiliwa na tatizo kubwa la kutokuwa na vifaa saidizi ambavyo vingewasaidia na kuwawezesha katika shughuli zao za kila siku.

Vivile akabainisha kuwa mwaka  2015, Tanzania ilikuwa moja ya wadhamini wa kuuwa Azimio kuhusu watu wenye ualibino, azimio ambalo pamoja na mambo mengine limelenga katika kutafuta ufumbuzi wa baadhi ya changamoto zinazo wakabili watu wenye ualibino katika maeneo mbalimbali yakiwamo ya elimu, afya na ajira.

“ Bila ya kuwa na vifaa saidizi watu wenye ulemavu wa aina yeyote  ile wanashindwa kupata fursa anuai ambazo kwao zingewawezesha kuishi pasipo utegemezi na hivyo kuchangia katika maisha yao binafsi na maendeleo ya nchi yao” akasisitiza Naibu Waziri. Na akatumia fursa hiyo kwa kuhimiza upatikanaji wa vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu ili waweze kujitegemea.

Awali akifungua mkutano wa tisa wa Mkataba wa Watu Wenye ulemavu,  Rais wa Baraza Kuu la  Umoja wa Mataifa,  Bw. Mogens Lykketoft, amesema nchi ambazo zimeridhia mkataba huo zinao wajibu wakuchukua hatua zote muhimu zikiwamo za maendeleo jumuishi kwa watu wenye ulemavu.

“Kila nchi mwanachama wa mkataba huu na asiye mwanachama ana kazi ya kufanya, lakini katika dunia ya leo mafanikio hayamo katika mikono ya serikali peke yake” akasisitiza Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.  

Na kwasababu hiyo, ametoa wito kwa serikali zote pamoja na wadau mbalimbali kufanya kazi kwa pamoja kwa lengo la kuwawezesha watu wenye ulemavu zaidi ya bilioni moja.

Pamoja na hotuba kutoka kwa nchi wanachama, mkutano huu ambao ni wa siku tatu utakuwa na mijadala pembeni yenye mada tofauti. Mkutano huo pia  unashirikisha Asasi zisizo za kiserikali zinazojihusisha na masuala ya watu wenye ulemavu.

Katibu Mkuu Mambo ya Nje ashiriki Warsha ya Makatibu Wakuu


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Aziz P. Mlima ( wa nne kutoka kulia waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Balozi Liberat Mfumukeko (wa nne kutoka kushoto), Makatibu Wakuu kutoka Wizara zinazosimamia masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na wataalam kutoka Sekretariati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika Warsha (Retreat) ya Makatibu Wakuu inayoendelea Mjini Moshi.

Monday, June 13, 2016

KATIBU MKUU AKIWA KWENYE SHEREHE ZA KUFUNGA MAFUNZO MAALUM YA JKT

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt Aziz P. Mlima akikagua gwaride liliondaliwa wakati wa sherehe za kufunga mafunzo maalum ya JKT kwaajili ya watumishi 30 walioajiriwa hivi karibuni.
Mmoja wa wahitimu wa mafunzo maalum ya JKT akitoa salaam maalum ya kijeshi kwa Katibu Mkuu Dkt. Aziz P. Mlima
Katibu Mkuu  Dkt Aziz P. Mlima akimpongeza mmoja wa wahitimu waliofanya vizuri zaidi wakati wa mafunzo maalum ya JKT

Waziri Mahiga amuaga rasmi Balozi wa Italia hapa nchini.

 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb), akimkabidhi zawadi Balozi wa Italia aliyemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini, Mhe. Luigi Scotto, katika hafla maalumu ya kumuaga iliyofanyika tarehe 10-06-2016, kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.


 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb), akimkabidhi zawadi Balozi wa Vatcan na mwakilishi wa Papa hapa nchini, Balozi Francisco Montecillo Padilla. Balozi Francisco alipewa zawadi hiyo kwenye hafla maalumu ya kumuaga Balozi wa Italia hapa nchini, iliyofanyika tarehe 10-06-2016, katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

 Waziri Mahiga akifurahia jambo na Balozi Padilla na Balozi Scotto, mara tu baada ya kuwapa zawadi.

Saturday, June 11, 2016

Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia akutana na viongozi wakuu wa Kamisheni ya Utalii na Wanyamapori mjini Riyadh

Balozi Hemedi Iddi Mgaza akiwa Ofisini kwa Kiongozi Mkuu wa Kamisheni ya Utalii ya Saudi Arabia, Mwanamfalme HRH Sultan bin Salman bin Abdulazizi kwenye mazungumzo ya ushirikiano.

Friday, June 10, 2016

Waziri Mahiga ashiriki maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya Kimbari ya nchini Rwanda dhidi ya Watutsi


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiongea na wageni waalikwa (hawapo pichani) katika maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994, maadhimisho hayo yaliandaliwa na Ubalozi wa Rwanda nchini Tanzania na kufanyika leo katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.
Katika hotuba yake alitoa wito kwa mataifa yote kuweka mbele suala la amani ili kuepuka kupoteza maisha ya wananchi wasio na hatia ambao ni nguvu kazi ya Taifa katika kujiletea maendeleo.

Naibu Waziri Kigwangalla ashiriki Mkutano wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu UKIMWI


 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,  Jinsia, Wazee na  Watoto,  Mhe. Dkt. Hamis Kigwangalla ( Mb) akizungumza   kwa niaba ya serikali kuhusu  mafanikio na changamoto ambazo  serikali imekuwa ikikabiliana nazo  dhidi ya  ugonjwa wa UKIMWI  katika Mkutano wa ngazi ya juu  wa Baraza Kuu la  Umoja wa  Mataifa kuhusu UKIMWI unaoendelea Umoja wa Mataifa New York-Marekani.

Waziri Mahiga ampokea Mjumbe Maalum kutoka Eritrea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Eritrea, Mhe. Isaias Afwerki kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli. Ujumbe huo  uliwasilishwa na Mjumbe Maalum  ambaye pia ni Balozi wa Eritrea nchini mwenye makazi Nairobi, Kenya, Mhe. Beyene  Russom Habtai.

Balozi wa Tanzania nchini Kuwait amtembelea Mkuu wa Itifaki nchini humo

Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim, Balozi wa Tanzania nchini Kuwait akiwa katika mazungumzo  na Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Kuwait, Mhe. Balozi Dhari Ajran Al-Ajran alipomtembelea Ofisini kwake kwa ajili ya kumshukuru kwa mchango wake binafsi pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje ya Kuwait katika kufanikisha juhudi za Tanzania kufungua Ubalozi wake nchini humo. Kadhalika, Mhe. Maalim alimuhakikishia Mhe. Al-Ajran utayari wa Tanzania katika kuhakikisha mahusiano baina yake na Kuwait katika nyanja za kisiasa, kiuchumi na kijamii yanasonga mbele zaidi.

Thursday, June 9, 2016

Wizara ya Mambo ya Nje yafanya mkutano na Vyombo vya Habari


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Ambapo alizungumzia juu ya biashara haramu ya binadamu ambayo imekuwa ikiendendeshwa na mtandao wa watu wasiowaaminifu kwa kuwalaghai mabinti wa Kitanzania kwa kuwaahidi kuwapa ajira nje ya nchi.kwenye mkutano uliofanyika leo katika ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.