Friday, June 10, 2016

Balozi wa Tanzania nchini Kuwait amtembelea Mkuu wa Itifaki nchini humo

Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim, Balozi wa Tanzania nchini Kuwait akiwa katika mazungumzo  na Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Kuwait, Mhe. Balozi Dhari Ajran Al-Ajran alipomtembelea Ofisini kwake kwa ajili ya kumshukuru kwa mchango wake binafsi pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje ya Kuwait katika kufanikisha juhudi za Tanzania kufungua Ubalozi wake nchini humo. Kadhalika, Mhe. Maalim alimuhakikishia Mhe. Al-Ajran utayari wa Tanzania katika kuhakikisha mahusiano baina yake na Kuwait katika nyanja za kisiasa, kiuchumi na kijamii yanasonga mbele zaidi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.