Friday, June 3, 2016

Wanachuo wa Royal Diffence College watembelea Wizara ya Mambo ya Nje.

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Edward Sokoine, akitoa maelezo ya awali wakati wa kuanza kwa mkutano na wanafunzi wa chuo cha Ulinzi cha Royal College of Diffence Studies kilichopo nchini Uingereza (hawapo pichani), ambao wapo kwenye ziara ya mafunzo katika nchi za Tanzania, Ethiopia na Malawi kwa ajili ya kubadilishana mawazo namna masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa yanayoibuka hivi sasa yanavyoathiri utulivu, usalama na ustawi wa nchi, kanda na dunia kwa ujumla. Mwingine katika picha ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Samuel Shelukindo.
Baadhi ya wanachuo hao wakisikiliza maelezo kutoka kwa mzungumzaji meza kuu (hayupo pichani). Masuala mbalimbali yalijadiliwa ikiwa ni pamoja na hali ya usalama katika eneo la nchi za maziwa makuu, nafasi ya wakuu wa nchi za Afrika katika utatuzi wa migogoro, uhusiano wa Tanzania na nchi jirani na mikakati ya kukabiliana na ugaidi katika kanda na dunia kwa ujumla.
Baadhi ya wanachuo pamoja na Askari wa JWTZ (waliovaa sare), wakisikiliza maelezo kutoka kwa mzungumzaji meza kuu (hayupo pichani).
 
Baadhi ya Maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia kwa makini mazungumzo.Wa kwanza kutoka kulia ni Bi. Olivia Maboko, Bi. Lilian Kimaro na Bi. Mona Mahecha
Mmoja wa wanachuo hao akiuliza swali.

Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samuel Shelukindo akiendelea kufafanua jambo katika mkutano huo.
 
Kikao kikiendelea...
 Balozi Sokoine, akifafanua jambo.
Kikao kikiendelea.
======================
PICHA NA: REUBEN MCHOME.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.