Thursday, June 2, 2016

Waziri Mahiga apokea Ujumbe Maalumu kutoka kwa Rais wa Angola.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt, Augustine Mahiga (Mb), akimpokea Mjumbe Maalumu wa Rais wa Angola, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa nchi hiyo, Mhe. Manuel Domingos Augusto leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri Mahiga akisalimiana na Balozi wa Angola nchini Tanzania, Mhe.Ambrosio Lukoki.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt, Augustine Mahiga (Mb), akiangalia bahasha iliyofungwa ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Angola Mhe. Jose Eduardo Dos Santos, baada ya kukabidhiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa nchi hiyo, Mhe. Manuel Domingos Augusto
 Waziri Mahiga akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo ambayo yalijikita zaidi kwenye masuala mbalimbali kuhusu Jumuiya ya Nchi za Maziwa Makuu.
Sehemu ya Ujumbe wa Angola ulioambatana na Mhe. Manuel Domingos Augusto, kulia ni Balozi wa Angola nchini Tanzania Mhe.Ambrosio Lukoki.
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samuel Shelukindo (kushoto), akifuatilia kwa makini mazungumzo hayo, pamoja na maofisa wa Wizara hiyo, Bi. Zulekha Tambwe (katikati) na Bw. Ally Kondo nao wakiendelea kurekodi kile kinachozungumzwa katika mazungumzo hayo.
                                                ==========================
Picha na Reuben Mchome.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.