Monday, June 6, 2016

Watafiti kuhusu masuala ya uchaguzi kutoka SADC wawasili nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Innocent Shiyo kulia akizungumza na Mtafiti kutoka SADC Bi. Patience Zonge raia wa Jamhuri ya Zimbabwe, ambaye  alitembelea katika ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa ajili ya kujitambulisha kabla ya kuanza rasmi tathmini ya shughuli za Baraza la Ushauri kuhusu masuala ya Uchaguzi la SADC. Tathmini hiyo inafanyika kufuatia agizo la Kamati ya Mawaziri lililotolewa katika kikao cha 17 kilichofanyika tarehe 20 hadi 21 Julai, 2015 ambapo nchini Tanzania tathmini hiyo itafanyika kati ya tarehe 6-7 Juni, 2016.
Sehemu ya wajumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea, kutoka kushoto ni Bw. Revocatus L. Ouko na Bw.Mohamed Kamal Mohamed.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.