Thursday, June 2, 2016

Mhe. Kairuki afungua Mkutano kuhusu Utawala wa Sheria

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mhe. Angella Kairuki (Mb), akitoa hotuba wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano wa ngazi ya Mawaziri wa nchi za Afrika kuhusu Utawala wa Sheria ulioandaliwa kwa ushirikiano kati ya Taasisi ya Sheria ya Kimataifa  (IDLO) na Serikali ya Tanzania na kufanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 01 na 02 Juni 2016.  Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Bi. Irene Khan. Waziri Kairuki alikuwa Mgeni Rasmi katika  Mkutano huo unaojadili nafasi ya Sheria katika kufikia Agenda ya Maendeleo Endelevu ya mwaka 2030 na Agenda ya AU ya mwaka 2063

Mhe.  Kairuki (Mb), wa pili kutoka kulia akiwa pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete wa kwanza kulia, Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mhe. Benjamin William Mkapa wa kwanza kushoto na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kimataifa ya Sheria (International Development Law Organization - IDLO), Bi. Irene Khan. Mhe. Mkapa na Mhe. Kikwete walikuwa wazungumzaji wakuu kwenye mkutano huo.     
Rais Mstaafu, Mhe. Benjamin Mkapa akiongea kwenye mkutano huo.
Rais Mstaafu, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete naye akiongea katika mkutano huo
Sehemu ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia mkutano
Mhe. Rais Mstaafu Kikwete akifuatilia mkutano, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi  wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Elisha Suku.
Wajumbe wa mkutano wakisikiliza hotuba  za ufunguzi wa Mkutano wa IDLO 
Sehemu nyingine ya ujumbe wa mkutano ambao ni Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini
Mhe. Mkapa akibadilishana mawazo na baadhi ya wajumbe wa mkutano mara baada ya shughuli ya ufunguzi kukamilika
Kutoka kulia ni Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Bi. Irene Khan na Mhe. Benjamin Mkapa wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukamilika kwa shughuli za ufunguzi
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete wa pili kutoka kulia akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Elizabeth wa kwanza kulia, Bi. Hamida Makame na Bw. Gerlad Mbwafu.


Picha ya pamoja kati ya Mgeni Rasmi, Mhe. Kairuki na wajumbe wa mkutano
Mhe. Kairuki akifafanua masuala mbalimbali kuhusu mkutano wa IDLO mbele ya waandishi wa habari.

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.