Thursday, June 2, 2016

Balozi Dora Msechu akutana na wafanyabiashara wa Sweden kuhamasisha biashara na uwekezaji.

Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Dora Msechu amefanya mkutano na wafanyabiashara wa Sweden ulioandaliwa na Baraza la Biashara la Sweden na Afrika Mashariki(SWEACC). 
 Mhe.Balozi Dora Msechu amewahamasisha Wafanyabiashara wa Sweden kuwekeza nchini Tanzania kwa kuwaeleza kwa kina fursa zilizopo pamoja na juhudi mahsusi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji na kukuza uchumi wa nchi ikiwa ni pamoja na mikakati kabambe ya kuimarisha sekta ya viwanda na kuboresha miundombinu.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.