Thursday, June 16, 2016

Katibu Mkuu Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akutana na Balozi wa Sweden nchini


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini Mhe. Balozi Katarina Rangnitt alipomtembelea  Wizarani, Juni 13, 2016.

 Balozi Dkt. Aziz Mlima na Mhe. Katarina Rangnitt wakiwasikiliza Mkurugenzi Mkazi wa TMEA (Trade Mark East Africa) Dkt. Josaphat Kweka ( wa kwanza kushoto kwa Balozi), Bi Sara Spant kutoka  Ubalozi wa Sweden na Bw. Ulf Ekdahl kutoka  Shirika la Maendeleo la Sweden (SIDA) katika Mkutano uliofanyika Wizarani Juni 13,2016

Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz Mlima na Mhe. Balozi Katarina Rangnit wakijadiliana jambo kwenye Mkutano uliofanyika Juni 13, 2016, Wizarani, wanaofuatilia kulia ni  Wakurugenzi  kutoka Wizarani Bw. Geoffrey Mwambe, Bw. Oswald Kyamani na Bw. Eliabi Chodota.

Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz Mlima, Mhe. Balozi Katarina Rangnit , Mkurugenzi  Mkazi wa TMEA, Maafisa wa Ubalozi wa Sweden na  Wakurugenzi kutoka Wizarani katika picha ya pamoja baada ya Mkutano June 13,2016

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.