Thursday, June 2, 2016

Waziri Mahiga ahitimisha Mkutano kuhusu Utawala wa Sheria

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), akitoa hotuba wakati wa kufunga rasmi Mkutano wa Kimataifa kuhusu masuala ya Utawala wa Sheria uliofanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 1 na 2 Juni, 2016 na kuwahusisha Mawaziri kutoka nchi za Afrika. Katika hotuba yake Mhe. Mahiga alisisitiza kuwa Tanzania itaendelea kupambana na rushwa ambaye ni adui mkubwa wa haki na usawa ili kuimarisha utawala wa sheria
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Baraka Luvanda akifuatilia hotuba ya Mhe. Waziri Mahiga (hayupo pichani)
Bi. Irene Khan, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kimataifa ya Sheria (IDLO) ambao ndio waandaaji wa mkutano huo kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania nae akichangia jambo wakati wa kumalizika kwa mkutano huo.
Waziri Mahiga akiwa na Balozi wa Italia hapa nchini, Mhe. Luigi Scotto (katikati) pamoja na Afisa katika Ubalozi huo
Mhe. Waziri Mahiga akisalimiana na Afisa Mwandamizi kutoka Ubalozi wa Burundi hapa nchini
Waziri Mahiga akizungumza na waandishi wa habari
Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.