Thursday, September 15, 2016

Wizara ya Mambo ya Nje yaratibu matembezi ya hisani kuchangia waathirika wa tetemeko Kagera


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akizungumza kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari. Katika mkutano huo aliwaeleza kuhusu Matembezi ya Hisani yanayoandaliwa na Wizara kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kuchangia waathirika wa  Tetemeko la Ardhi lililotokea Mkoani Kagera hivi karibuni. Matembezi hayo yatafanyika tarehe 17 Septemba, 2016 Jijini Dar es Salaam. Pia aliwajulisha kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali kufuatia kutekwa kwa madereva wa malori huko DRC.
Mkutano na waandishi wa habari ukiendelea.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Madereva kutoka Tanzania watekwa nchini DRC.

Serikali imepokea taarifa za kutekwa kwa malori 12 katika eneo la Namoyo Jimbo la Kivu Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, jana tarehe 14 Septemba 2016. Kati ya malori hayo nane yanamilikiwa na mfanyabiashara wa Kitanzania, Bw. Azim Dewji na mengine yanamilikiwa na wafanyabiashara kutoka Kenya.


Kwa taarifa zilizopatikana watekaji ni kikundi cha waasi cha MaiMai ambao baada ya kuyateka magari hayo, waliwashusha madereva na kuwapeleka porini na kisha kuteketeza kwa moto malori manne ambayo yote ni ya Bw. Dewji. Waasi hao wametoa saa 24 kuanzia jana saa 10 jioni walipwe fedha kiasi cha Dola za Kimarekani 4,000 kwa kila dereva ili waweze kuwaachia. 

Wametishia kuwaua mateka hao endapo hawatalipwa kiasi hicho cha fedha wanachokitaka itakapofika saa 10 jioni leo. Katika tukio hilo, madereva wawili wa Kitanzania wamefanikiwa kutoroka ambao ndio waliosaidia kutoa taarifa rasmi kuhusu tukio hilo.


Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeshachukua hatua za awali za kuwasiliana na Serikali ya DRC ili kuhakikisha kuwa madereva hao wanaachiwa haraka iwezekanavyo wakiwa salama kabisa.


Tukio hili ni la pili kutokea katika miaka ya hivi karibuni ambapo mwaka 2015 Mashekhe kutoka Tanzania walitekwa nchini DRC lakini kwa ushirikiano wa Serikali hizi mbili zilifanikisha mashekhe hao kuachiwa huru bila madhara yoyote.


Serikali ingependa kuushauri Umma wa Watanzania hususan wafanyabiashara kuomba taarifa ya hali ya usalama kwa maeneo yenye matatizo ya kiusalama kama Mashariki ya Congo hususan Kivu ya Kusini kabla ya kusafiri kwenda maeneo hayo.



Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Dar es Salaam, 15 Septemba 2016.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje afungua Kongamano la Kimataifa la Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan A. Kolimba (katikati) pamoja na meza kuu wakitoa heshima wakati Wimbo wa Taifa ukiimbwa kwenye ufunguzi wa kongamano la Kimataifa la Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki (CHAKAMA) uliofanyika katika Ukumbi wa Nkurumah, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Naibu Waziri, Mhe. Dkt. Susan A. Kolimba (kushoto) akifurahia jambo wakati wa ufunguzi wa kongamano la Kimataifa la CHAMAKA, kulia ni Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Florens D. A. M Luoga.
Mheshimiwa Dkt. Susan A. Kolimba akimpongeza mtunzi na mwimbaji wa mashairi Bw. Issa Ally.
 Mhe. Dkt. Susan A. Kolimba akitoa hotuba ya ufunguzi wa kongamano la CHAKAMA.
 Mhe. Dkt. Susan A. Kolimba akiwa akionesha kitabu kilichozinduliwa kwenye kongamano la Kiswahili la CHAKAMA kulia ni Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Florens D. A. M Luoga.
Sehemu ya wadau wa lugha ya kiswahili waliohudhuria kongamano la Kimataifa la CHAKAMA wakifuatilia jambo.
Meza kuu (walioketi) wakiwa katika picha ya pamoja na Wahadhiri wa chuo Kikuu cha Dar es Salaam.


Rais Magufuli amuapisha Balozi Dkt. Ramadhani Dau

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Ramadhani Dau kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia Ikulu jijini Dar es Salaam.

Wednesday, September 14, 2016

Wizara ya Mambo ya Nje yachangia waathirika wa tetemeko Mkoani Kagera

Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akipokea mfano wa hundi ya Shilingi milioni 10 kutoka kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (katikati) ikiwa ni mchango wa Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera hivi karibuni. Mkutano huo wa kuhamasisha uchangiaji  ulifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 13 Septemba, 2016 na kuwashirikisha Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini na Wafanyabiashara. Kushoto ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Charles Mwijage na kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Aziz Mlima
Sehemu ya Mabalozi na Wafanyabiashara walioshiriki mkutano huo
Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa akitoa hotuba wakati wa mkutano wa kuhamasisha uchangiaji kwa maafa yaliyotokea Kagera kufuatia tetemeko la ardhi.
Sehemu nyingine ya wafanyabiashara akiwemo Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Dkt. Reginald Mengi (wa kwanza kushoto)
Sehemu ya wageni waalikwa walioshiriki mkutano huo wakiwemo Wakurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Mhe. Dkt. Kolimba akitoa neno la ukaribisho wakati wa mkutano huo
Mwenyekiti wa TPSF, Dkt. Mengi akizungumza wakati wa mkutano huo
Mkutanoo ukiendelea


Tuesday, September 13, 2016

TAMKO (COMMUNIQUE); Mkutano wa Dharula wa 17 wa Viongozi Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

COMMUNIQUE: 17TH EXTRA-ORDINARY SUMMIT OF HEADs OF STATE OF THE EAST AFRICAN COMMUNITY
1. THE EAST AFRICAN COMMUNITY HEADS OF STATE, THEIR EXCELLENCIES PRESIDENT DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND CHAIRPERSON OF THE SUMMIT, PRESIDENT YOWERI KAGUTA MUSEVENI OF THE REPUBLIC OF UGANDA, PRESIDENT PAUL KAGAME OF THE REPUBLIC OF RWANDA, DEPUTY PRESIDENT WILLIAM RUTO OF THE REPUBLIC OF KENYA; AND AMB. ALAIN AIMÈ NYAMITWE, MINISTER OF EXTERNAL RELATIONS AND INTERNATIONAL COOPERATION OF THE REPUBLIC OF BURUNDI REPRESENTING PRESIDENT PIERRE NKURUZINZA HELD THE 17TH EXTRA-ORDINARY SUMMIT MEETING OF THE EAST AFRICAN COMMUNITY HEADS OF STATE ON 8TH SEPTEMBER, 2016 IN DAR ES SALAAM, TANZANIA. IN ATTENDANCE WERE H.E ALI MOHAMED SHEIN, PRESIDENT OF ZANZIBAR, AND HON AGGREY TISA SABUNI, SPECIAL ENVOY OF GENERAL SALVA KIIR MAYARDIT, PRESIDENT OF THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN.

2. THE HEADS OF STATE AND GOVERNMENT MET IN A WARM AND CORDIAL ATMOSPHERE.

3. THE HEADS OF STATE CONSIDERED A REPORT OF THE COUNCIL OF MINISTERS ON EU-EAC ECONOMIC PARTNERSHIP AGREEMENT (EPA) AND NOTED THAT TWO PARTNER STATES HAVE SIGNED THE EPA. THE SUMMIT REQUESTED FOR THREE MONTHS TO FINALISE ON THE CLARIFICATION OF THE CONCERNS OF SOME OF THE REMAINING PARTNER STATES BEFORE CONSIDERING THE SIGNATURE OF EPA AS A BLOC. THE SUMMIT CALLED UPON EU NOT TO PENALISE THE REPUBLIC OF KENYA AND DIRECTED THE SECRETARIAT TO COMMUNICATE TO EU ON THIS MATTER.

4. THE HEADS OF STATE RECEIVED A REPORT FROM H. E. BENJAMIN WILLIAM MKAPA, THE FACILITATOR OF THE INTER- BURUNDI DIALOGUE. THE SUMMIT ENDORSED ALL THE RECOMMENDATIONS AS PROPOSED IN H. E BENJAMIN WILLIAM MKAPA’S REPORT ON THE INTER BURUNDI DIALOGUE AND DIRECTED THE COUNCIL OF MINISTERS TO AVAIL A BUDGET FOR THE INTER BURUNDI DIALOGUE.

5. THE HEADS OF STATE RECEIVED A REPORT OF THE COUNCIL OF MINISTERS ON MATTERS RELATING TO THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN AND CONGRATULATED THE PEOPLE AND THE GOVERNMENT OF THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN FOR THE TIMELY DEPOSITING OF THE INSTRUMENTS OF RATIFICATION OF THE TREATY OF ACCESSION OF THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN INTO THE EAST AFRICAN COMMUNITY WITH THE SECRETARY GENERAL. THE HEADS OF STATE DIRECTED THE COUNCIL OF MINISTERS TO PRESENT THE ROADMAP FOR THE ACCELERATED INTEGRATION OF THE REPUBLIC OF SOUTH SUDAN INTO THE EAC AT THE 18TH SUMMIT OF THE EAC HEADS OF STATES SCHEDULED FOR NOVEMBER, 2016.

6. THE HEADS OF STATE RECEIVED THE REPORT OF THE 33RD EXTRA-ORDINARY MEETING OF THE COUNCIL OF MINISTERS RECOMMENDING TO THE SUMMIT THE APPOINTMENT OF HON. CHRISTOPHE BAZIVAMO FROM THE REPUBLIC OF RWANDA AS A DEPUTY SECRETARY GENERAL OF THE EAST AFRICAN COMMUNITY.

7. THE HEADS OF STATE APPOINTED HON. CHRISTOPHE BAZIVAMO AS DEPUTY SECRETARY GENERAL OF THE EAST AFRICAN COMMUNITY TO A THREE YEAR TERM WITH EFFECT FROM 8TH SEPTEMBER, 2016 AND PRESIDED OVER HIS SWEARING IN CEREMONY.

8. THEIR EXCELLENCIES PRESIDENT YOWERI KAGUTA MUSEVENI OF THE REPUBLIC OF UGANDA, PRESIDENT PAUL KAGAME OF THE REPUBLIC OF RWANDA, DEPUTY PRESIDENT WILLIAM RUTO OF THE REPUBLIC OF KENYA AND AMB. ALAIN AIMÉ NYAMITWE MINISTER OF EXTERNAL RELATIONS AND INTERNATIONAL COOPERATION OF THE REPUBLIC OF BURUNDI THANKED THEIR HOST, HIS EXCELLENCY PRESIDENT DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND CHAIRPERSON OF THE SUMMIT, FOR THE WARM AND CORDIAL HOSPITALITY EXTENDED TO THEM AND THEIR RESPECTIVE DELEGATIONS DURING THEIR STAY IN DAR ES SALAAM.


……………………........…....
H.E DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI
PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

…………….................……
H.E YOWERI KAGUTA MUSEVENI
PRESIDENT OF THE REPUBLIC OF UGANDA

…………………........…
H.E PAUL KAGAME
PRESIDENT OF THE REPUBLIC OF RWANDA

….………….……..…..…..
H.E WILLIAM RUTO
DEPUTY PRESIDENT OF THE REPUBLIC OF KENYA

……………………....…
AMB. ALAIN AIMÉ NYAMITWE
MINISTER OF EXTERNAL RELATIONS AND INTERNATIONAL COOPERATION
REPUBLIC OF BURUNDI


Friday, September 9, 2016

Mkutano wa 17 wa Dharura wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wamalizika Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza katika Mkutano wa 17 wa Viongozi Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akizungumza katika Mkutano wa 17 wa Viongozi Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Rwanda Mhe. Paul Kagame akizungumza katika Mkutano wa 17 wa Viongozi Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akizungumza katika Mkutano wa 17 wa Viongozi Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Ikulu, Jijini Dar es Salaam
Naibu Rais wa Kenya Mhe. William Ruto akizungumza katika Mkutano wa 17 wa Viongozi Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Ikulu Jijini Dar es Salam
Sehemu ya wageni waalikwa wakifuatilia Mkutano

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu Wengine wa Nchi Wanachama wa Jumuiya na Wawakilishi.