Sehemu ya Maafisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo kati ya Dkt. Kolimba na Balozi Welbert |
Mazungumzo yakiendelea |
Naibu Waziri, Dkt. Susan Kolimba akiagana na Balozi Welbert mara baada ya kumaliza mazungumzo naye. |
Sehemu ya Maafisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo kati ya Dkt. Kolimba na Balozi Welbert |
Mazungumzo yakiendelea |
Naibu Waziri, Dkt. Susan Kolimba akiagana na Balozi Welbert mara baada ya kumaliza mazungumzo naye. |
Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga, Afisa Mambo ya Nje, Bw. Hangi Mgaka na Katibu wa Waziri, Bw. Gerald Mbwafu wakifuatilia mazungumzo. |
Mazungumzo yakiendelea |
Picha ya pamoja. |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Bi. Hawa Dabo alipomtembelea leo katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam. |
Waziri Mahiga akiendela na mazungumzo na Bi. Gabo huku Bi. Ngusekela Nyerere (kulia), Afisa Mambo ya Nje akinukuu. |
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Aziz P. Mlima, akifungua Mkutano cha Makatibu Wakuu nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa Kamati Ndogo ya Mawaziri ya Siasa na Diplomasia ya SADC (Inter State Politics and Diplomacy Sub Committee-ISPDC) unaotarajiwa kufanyika tarehe 23 na 24 Februari, 2017. Mkutano wa Makatibu Wakuu unafanyika kwa siku mbili katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. |
Sehemu ya wajumbe wa Mkutano kutoka katika mataifa ya nchi wanachama wakifuatilia mkutano. |
Kaimu Mkuu wa Mabalozi Mhe. Balozi Edzai Chimonyo (wa kwanza kushoto) na wajumbe wengine wakifuatilia mkutano. |
Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Dkt. Stergomena Tax (wa pili kushoto) na wa kwanza kulia ni Balozi Simba Yahya, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakifuatilia mkutano. |
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia Mkutano. |
Balozi wa Tanzania kwenye Muungano wa Visiwa vya Comoro, Mhe. Chabaka Kilumanga akitunukiwa Nishani ya Juu (highest civilian honor) na Rais wa nchi hiyo, Mhe. Azali Assoumani hivi karibuni. |
Nishani hiyo imetolewa na Mhe Azali kwa kutambua mchango wa Balozi Kilumanga katika kudumisha uhusiano mzuri uliopo baina ya Tanzania na Comoro, pamoja na kumpongeza kwa utumishi uliotukuka. |
Hafla hiyo ilifanyika Ikulu ya
Comoro kwa ajili ya kumuaga Balozi Kilumanga baada ya kumaliza muda wake wa
kazi nchini humo
|
Mhe. Rais Azali (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Kilumanga na Mkewe |
Balozi Kilumanga akipongezwa na Mkuu wa Utawala Ubalozini, Bw. Mudrick Soragha mara baada ya kutunikiwa nishani na Rais wa Comoro |
Balozi wa Tanzania nchini Brazil,
Mhe. Emmanuel Nchimbi akianza rasmi majukumu yake ya ofisini kwenye wadhifa wa Balozi mara baada ya kuwasili
rasmi kwenye Ofisi za Ubalozi wa Tanzania zilizopo kwenye makao makuu nchini
humo, mjini Brasilia.
|
Balozi Nchimbi akiwa kwenye picha
ya pamoja na Maafisa wa Ubalozi
wa Tanzania nchini Brazil mara baada ya kumpokea na kumkaribisha rasmi kituoni hapo.
|
Balozi Nchimbi (kushoto) akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Mambo ya Nje ya Brazil mara baada ya kuwasili Wizarani hapo kwa utambulisho. |
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba akizungumza na Balozi Mteule wa Oman nchini, Mhe. Ali Abdullah Al Mahruqi alipomtembelea Wizarani leo, Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika masuala ya ushirikiano na juu ya ukamilishaji wa makubaliano ya kibiashara na uwekezaji ili kuweza kunufaika na ushirikiano wa kidiplomasia ambao umekuwa ukizidi kuimarika baina ya mataifa hayo mawili. |
Mhe. Al Mahruqi akimweleza Naibu Waziri mipango ya kiutendaji ya Ubalozi wa Oman nchini na jinsi Serikali yake ilivyojidhatiti katika kuhakikisha mahusiano yaliyopo yataelekeza nguvu zaidi katika kusimamia sekta zinazogusa kukuza uchumi wa wananchi. |
Mhe. Al Mahruqi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi za Wizara, kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Abdallah Kilima. |
Picha ya pamoja wakiagana mara baada ya mazungumzo. |
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Abdallah Kilima (kulia) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi Mteule wa Oman hapa nchini, Mhe. Ali Abdullah Al Mahruqi. Mazungumzo yao yalijikita katika kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na Oman kwenye sekta mbalimbali zikiwemo biashara, elimu na afya. Pamoja na hayo Balozi Kilima amemuahidi Balozi kumpatia ushirikiano wa kutosha kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wowote katika kutekeleza majukumu yake hapa nchini. |
Mkutano ukiendelea.Kulia ni Afisa Mambo ya Nje, Bw. Odilo Fidelis |
Balozi Kilima akiagana na Balozi Mteule Ali Abdullah Al Mahruqi mara baada ya mazungumzo yao. |
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba (Mb.), amezungumza na waandishi wa habari, kufafanua suala la Watanzania waliopata matatizo ya kufukuzwa nchini Msumbiji. Pia alitumia fursa hiyo kuwaomba Watanzania wote wanaosafiri kwenye nchi nyingine kuhakikisha wanafuata sheria na taratibu ikiwemo kupata vibali halali vya kukaa kwenye nchi husika. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika na Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Innocent Shiyo na kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Mindi Kasiga. |
Sehemu ya waandishi wa habari wakimsikiliza Dkt. Kolimba (hayupo pichani), alipokuwa akizngumza nao. |
Mkutano na waandishi wa habari ukiendelea. ==================================================
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Taarifa kuhusu Watanzania waliopata
matatizo nchini Msumbiji
Tumepokea taarifa za kukamatwa na kufukuzwa kwa raia wa Tanzania
waliokuwa wakiishi katika mji wa Monte Puez ulio Cabo Delgado, Jamhuri ya
Msumbiji.
Serikali ya Msumbiji imekiri kuwepo kwa operesheni maalum ya kuwakamata
na kuwarudisha raia wa nchi za kigeni wanaoishi katika mji huo bila kufuata
Sheria za Uhamiaji za nchi hiyo. Aidha, Serikali hiyo imetaarifu kwamba, zoezi
hilo limeanzia mji wa Monte Puez kwa kuwa una raia wengi wa kigeni
ikilinganishwa na miji mingine.
Kufuatia hali hiyo, Ubalozi wetu nchini Msumbiji upo eneo la tukio ili
kufuatilia suala hili na mamlaka husika. Aidha, unaendelea kufanya mawasiliano
ya Kidiplomasia na Serikali ya Msumbiji ili kuhakikisha usalama wa Watanzania
na mali zao, unapewa kipaumbele. Inakadiriwa kuwa Watanzania wapatao elfu tatu
(3,000) wanaishi na kufanya shughuli za kiuchumi na kijamii katika mji huo wa
Monte Puez.
Kuanzia zoezi hilo lilipoanza, Raia wa Tanzania wapatao 132
wamesharudishwa nchini. Tarehe 11/02/2017 walirejeshwa raia 58. Tarehe
14/02/2017 wamerejeshwa raia 24 na leo tarehe 15/02/2017 wamesharejeshwa raia
50.
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inawahakikishia
Watanzania kuwa uhusiano kati ya Tanzania na jirani yetu Msumbiji ni mzuri, na
hivyo itafanya kila jitihada kuhakikisha hali ya usalama wa Watanzania na
biashara zao, inarudi kuwa shwari na kwa wakati. Mwezi Desemba 2016, Tanzania
na Msumbiji zilifanya mkutano wa ujirani mwema uliolenga kuimarisha ushirikiano.
Mkutano huo uliofanyika kwenye mji wa Pemba, Cabo Delgado uliainisha maeneo ya
ushirikiano yakiwemo masuala ya biashara na uhamiaji.
Serikali inaendelea kuwakumbusha Watanzania waishio ughaibuni, kufuata
Sheria na taratibu za nchi hizo, ikiwemo kuwa na vibali halali vya makazi na
biashara.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki
15 Februari, 2017
|