Thursday, February 16, 2017

Mkurugenzi wa Mashariki ya Kati akutana kwa mazungumzo na Balozi Mteule wa Oman nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Abdallah Kilima (kulia) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi Mteule wa Oman hapa nchini, Mhe. Ali Abdullah Al Mahruqi. Mazungumzo yao yalijikita katika kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na Oman kwenye sekta mbalimbali zikiwemo biashara, elimu na afya. Pamoja na hayo Balozi Kilima amemuahidi Balozi kumpatia ushirikiano wa kutosha kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wowote katika kutekeleza majukumu yake hapa nchini.
Mkutano ukiendelea.Kulia ni Afisa Mambo ya Nje, Bw. Odilo Fidelis


Balozi Kilima akiagana na  Balozi Mteule Ali Abdullah Al Mahruqi mara baada ya mazungumzo yao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.