Sunday, February 26, 2017

Rais Museveni amaliza ziara yake nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili hapa nchini.
Rais Museveni akiagana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga. Kushoto ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (Mb.). Kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi John Kijazi.
Rais Museveni akiagana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Innocent Shiyo.
Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Bw. Elibariki Maleko akiagana na Rais Museveni
Rais Museveni akipunga mkono wa kwa heri kwa Rais Magufuli na Viongozi wengine walioshiriki kumuaga mara baada ya kumaliza ziara yake nchini.
Kutoka kulia ni Balozi wa Uganda nchini Mhe. Dorothy Hyuha, Balozi Shiyo, Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin, Mnikulu, Bw. Ngusa Samike na Balozi Zuhura Bundala, Mshauri wa Rais Masuala ya Diplomasia wakimuaga Rais Museveni (hayupo pichani) mara baada ya kumaliza ziara yake nchini.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.