Wednesday, February 15, 2017

Naibu Waziri Mambo ya Nje akutana na Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo wa Korea



Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba akizungumza na Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo wa Jamhuri ya Korea,Mhe. Balozi Choi Jong-moon, ambaye amewasili nchini kwa ziara ya siku mbili inayotarajiwa kumalizika tarehe 15 Februari, 2017.
Mhe. Balozi Jong-moon  akizungumza na Mhe. Dkt. Kolimba, ambapo pamoja na masuala ya ushirikiano alieleza nia ya Serikali ya Jamhuri ya Korea katika kuongeza maeneo ya ushirikiano hususan katika Ujenzi wa Miundombinu, Elimu, Utalii, biashara na Uwekezaji.
Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Justa Nyange, Mkurugenzi msaidizi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Deus Kaganda na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Bertha Makilagi.
Wa kwanza kulia ni Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mhe. Song Geum Yong pamoja na maafisa wa Ubalozi  ambao waliambatana na Mhe. Jong-moon, wakifuatilia mazungumzo.
Mazungumzo yakiendelea.
Wakiagana mara baada ya mazungumzo.
Picha ya pamoja Manaibu Waziri na wajumbe kutoka Serikali ya Tanzania na Korea.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.