Thursday, February 9, 2017

Chuo cha Diplomasia chapokea ufadhili wa Kompyuta 150 kutoka Serikali ya Korea


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Diplomasia Mhe. Balozi Ombeni Sefue (katikati) wakipokea kompyuta kutoka kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum Young.
Hafla ya makabidhiano hayo ilifanyika tarehe 8 Februari, 2017 chuo cha Diplomasia Kurasini Jijini Dar es Salaam

Mhe. Balozi Sefue akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Bodi na Uongozi wa Chuo cha Diplomasia mara baada ya kupokea ufadhili huo kutoka kwa Serikali ya Jamhuri ya Korea.
Balozi Mwinyi akizungumza kwa niaba ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambapo aliipongeza Serikali ya Jamhuri ya Korea kwa kuendelea kuwa mdau wa maendeleo katika sekta mbalimbali nchini hususan sekta ya Elimu.



Sehemu ya Wakufunzi wa Chuo cha Diplomasia wakimsikiliza Balozi Sefue (hayupo pichani) wakati alipokuwa anatoa neno la shukrani.
Sehemu nyingine ya watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakishuhudia makabidhiano.
Makamu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia, Dkt. Bernard Archiula (wa kwanza kushoto), akifafanua jambo kwa Balozi Sefue na Balozi Mwinyi.
Balozi Ombeni Sefue akizungumza na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Mindi Kasiga.
Wakiwa katika picha ya pamoja.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.