Sunday, February 12, 2017

Rais Magufuli awaapisha Mabalozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Uganda na Algeria

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Mhe. Joseph Edward Sokoine. Hafla za uapisho huo zimefanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Rais Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Balozi Sokoine.

Mhe. Rais Magufuli akimuapisha Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Grace Aaron Mgovano.
Mhe. Rais Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Balozi Mgovano.

Mhe. Rais Magufuli akimuapisha Balozi wa kwanza wa Tanzia nchini Algeria, Mhe. Omar Yussuf Mzee.

Mhe. Rais Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Balozi Mzee

Waheshimiwa Mabalozi wakila kiapo cha Maadili ya Viongozi wa Umma, pembeni yao ni Kamishna Mkuu wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala (wa kwanza kulia)  na  Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Bw. Rogers William Sianga ( wa pili kutoka kulia) ambao pia waliapishwa pamoja na Waheshimiwa Mabalozi.

Kutoka kulia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa na Kaimu Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Hamis Juma wakishuhudia hafla ya kuapishwa kwa waheshimiwa Mabalozi na Makamishna Wakuu wa Uhamiaji na Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya.

Sehemu ya Waheshimiwa Mawaziri, Manaibu Waziri, viongozi waandamizi kutoka katika wizara mbalimbali na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Bw. Paul Makonda wakifuatilia hafla ya kuapishwa. 

Sehemu nyingine ya Mawaziri na viongozi wa Mamlaka ya kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya wakifuatilia hafla ya uapisho, wa pili kutoka kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb). 

Hafla ikiendelea, wa pili kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Mhe. Dkt. Susan Kolimba (Mb).

Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakishuhudia kuapishwa kwa mabalozi na Makamishna Wakuu, Kutoka Kulia ni Balozi Innocent Shio, Balozi Abdallah Kilima na Balozi Anisa Mbega. 

Sehemu nyingine ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa Ikulu katika hafla ya kuapishwa kwa Mabalozi na Makamishna Wakuu, Kutoka kushoto ni Bw. Osward Kyamani, Bw. Bernard Haule na Bw. Nigel Msangi.

Picha ya pamoja meza kuu, Waheshimiwa Mabalozi na Makamishna Wakuu walioapishwa .

Picha ya pamoja meza kuu, Waheshimiwa Mabalozi na Makamishna Wakuu walioapishwa pamoja na Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.