Tuesday, February 7, 2017

Waziri Mahiga apokea nakala za hati za utambulisho za Mabalozi wateule wa Zambia na Cuba


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi mteule wa Zambia nchini Tanzania Mhe.Benson Keith Chali alipowasili Wizarani Jijini Dar es Salaam kukabidhi nakala za hati za utambulisho

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga akipokea hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Zambia nchini Tanzania Mhe. Chali

Waziri Mhe.Balozi Dkt. Mahiga na Balozi Mteule wa Zambia nchini Mhe. Chali wakiwa katika picha ya pamoja. Wa pili kulia ni Mkuu wa Itifaki Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Grace Martin, wa kwanza kulia ni Afisa kutoka Wizarani na kushoto ni Maafisa kutoka Ofisi za Ubalozi wa Zambia nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa Cuba nchini Tanzania Mhe.Lucas Domingo Harnandez Pelledo mara baada ya kuwasili Wizarani kuwasilisha nakala za hati za utambulisho

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea nakala za hati za utambulisho kutoka Balozi Mteule wa Cuba nchini Tanzania Mhe.Lucas Domingo Harnandez Pelledo

Picha ya pamoja


Aidha, Waziri Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga amekutana na kufanya mazungumzo na  Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi Wizarani Jijini Dar es Salaam mapema leo asubuhi.Katika mazungumzo hayo wamejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano wa kidiplomasia, uchumi na kijamii baina ya nchi hizi mbili Tanzania na Burundi


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi Mhe. Alain Aime Nyamitwe walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam



Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga akizungumza


Waziri  Mhe. Mahiga akimsiliza Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi Mhe. Alain Aime Nyamitwe walipokuna kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.