Monday, February 6, 2017

Rais Magufuli awaapisha Mabalozi wa Tanzania nchini Ufaransa na DRC

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimwapisha Balozi wa Tanzania Ufaransa Mhe.Samuel W. Shelukindo.
Sherehe za uapisho huo zimefanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Mhe. Rais Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Balozi Shelukindo.
Mhe. Rais Magufuli akimuapisha Luteni mstaafu Paul Ignace Mella kuwa Balozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Mhe. Rais Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Balozi Mella.
Kutoka kulia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Hamis Juma na Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Janeth Magufuli wakifuatilia hafla ya kuapishwa kwa Mabalozi na baadhi Wakuu wa Majeshi ya Ulinzi akiwemo Mkuu wa Jeshi ya Ulinzi nchini.
Kutoka kulia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba, Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Angella Kairuki pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Issa Haji Ussi Gavu wakifuatilia hafla ya uapisho. 
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima (wa pili kulia) akifuatilia sherehe za kuapishwa kwa Mabalozi na baadhi ya viongozi wa majeshi ya ulinzi. Pembeni yake  ni wageni waalikwa kutoka katika vyombo vya ulinzi wakifuatilia pia hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Idara ya  Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Anisa Mbega (wa kwanza kulia) akifuatiwa na  Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama Bw. Stephen Mbundi nao wakiwa Ikulu kwenye hafla ya kuapishwa Mabalozi
Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia hafla ya uapisho. Kutoka  kushoto ni Balozi Abdallah Kilima, Balozi Baraka Luvanda na Balozi Innocent Shio.
Sehemu ya viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wakifuatilia hafla ya kuapishwa kwa viongozi na Mabalozi
Mhe. Rais Magufuli akimpongeza Balozi Shelukindo mara baada ya kumalizika kwa tukio la kuapishwa.
Kushoto ni Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin pamoja na Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Geofrey Pinda wakiratibu shughuli za Itifaki.
Picha ya pamoja Mhe. Rais Magufuli na Mabalozi mara baada ya kuwaapisha.

Picha ya pamoja Mhe. Rais Magufuli, Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Shein, Mawaziri, viongozi waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Viongozi wa majeshi na Mabalozi walioapishwa, 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.