Saturday, February 25, 2017

Tanzania yaahidi kuimarisha Diplomasia ya Uchumi na Uganda

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam wakati wa ziara ya Rais wa Uganda hapa nchini, Mhe. Yoweri Museveni (anayeonekana ameketi kulia). Katika hotuba yake Rais Magufuli aliahidi kuimarisha urafiki na undugu uliodumu kwa miaka mingi baina ya mataifa hayo mawili.
Mhe. Rais Museveni nae akihutubia katika mkutano na waandishi wa habari wakati wa ziara yake nchini.
 Pamoja na kuzungumzia masuala ya ushirikiano wa kidiplomasia, Rais Museveni aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuikomboa  Uganda dhidi ya adui Nduli Idd Amin Dada na ukombozi wa kiuchumi kwa kujenga reli ya kati " standard gauge" ambayo itaenda sambamba na ujenzi wa bandari kavu "Dry Port" Jijini Mwanza ili kurahisisha usafirishaji wa mizigo ya Uganda kutoka Bandari ya Dar es Salaam. 
Sehemu ya Mawaziri na Maafisa Waandamizi wa Serikali ya Tanzania waliohudhuria mkutano huo ambao ulitanguliwa na hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ushirikiano katika masuala ya Siasa na Diplomasia. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia masuala ya Kimataifa wa Uganda, Mhe. Okello Oryem wakisaini Mkataba wa Ushirikiano katika masuala ya Siasa na Diplomasia.
Wakibadilishana mkataba mara baada ya kuusaini.
Marais wakipongezana mara baada ya kutoa hotuba.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.