Friday, February 24, 2017

Waziri Mahiga aongoza maadhimisho ya siku ya Taifa la Kuwait

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akizungumza katika hafla ya kuadhimisha siku ya Taifa la Kuwait. Katika hafla hiyo Dkt. Mahiga ambaye alikuwa mgeni rasmi alitumia fursa hiyo kulipongeza taifa hilo na kuahidi kuendeleza ushirikiano  uliopo kati ya Tanzania na Kuwait.Pia alimpongeza Balozi wa Kuwait hapa nchini Mhe. Jasem Ibrahim Al Najem kwa juhudi zake za kuboresha na kukuza ushirikiano kati ya Tanzania na Kuwait hususan kwa kuchangia  sekta mbalimbali zikiwemo huduma za kijamii kama elimu na afya. Hafla  hiyo iliyonyika katika Hoteli ya Hyatt Jijini Dar es Salaam
Dkt. Mahiga akiendelea kuzungumza huku wageni waalikwa wakimsikiliza
Balozi wa Kuwait hapa nchini Mhe. Jasem Ibrahim Al Najem nae akizungumza wakati wa hafla hiyo. 
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Abdallah Kilima pamoja na Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia hotuba mbalimbali zilizokuwa zikiendelea kutolewa na Waziri Mahiga na Balozi Jasem Ibrahim Al Najem
Dkt. Mahiga, Rais Mstaafu Dkt. Mwinyi pamoja na Balozi Jasem Ibrahim Al Najem wakikata keki iliyoandaliwa maalum kwa ajili ya maadhimisho hayo.
Sehemu nyingine ya wageni waalikwa wakishuhudia zoezi hilo la ukataji keki likiendelea.
Balozi Al Najem akimwonyesha Dkt. Mahiga picha za miradi mbalimbali ambayo imekwisha fanyika na inayoendelea kufanyika kupitia Serikali ya Kuwait hapa nchini.
Dkt. Mwinyi akipokea picha yenye mchoro wa Swala kutoka kwa Balozi Al Najem
Dkt. Mahiga akipokea picha ya mchoro wa Twiga kutoka kwa Balozi Al Najem
Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.